1 Samweli 13:22 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
22 Kwa hiyo, siku ya vita hakuna mutu kati ya wote waliokuwa pamoja na Saulo na Yonatani aliyekuwa na upanga au mukuki isipokuwa Saulo na mwana wake Yonatani.
Yule malaika akaniambia vilevile niseme neno hili la Yawe juu ya Zerubabeli: Hauwezi kushinda kwa nguvu au kwa uwezo wako mwenyewe, lakini kwa musaada wa roho wangu. –Ni Yawe wa majeshi anayesema.
Lakini sisi tunaokuwa na hazina hii ya kiroho, tuko vyombo vya udongo, kusudi watu waone waziwazi uwezo huu wa ajabu sana unaotoka kwa Mungu lakini si kwetu sisi wenyewe.
Waisraeli walikuwa wanalipa feza sehemu mbili ya tatu za shekeli kwa kunoa majembe na sururu. Na bei ya kunoa shoka au kuchongoa chuma ilikuwa sehemu moja ya tatu ya shekeli.
Watu wote waliokusanyika hapa leo, watajua kwamba Yawe hahitaji mikuki kwa kuwaokoa watu. Hii ni vita ya Yawe, naye atawatia ninyi wote katika mikono yetu.”
Ndivyo Daudi alivyomushinda Goliati kwa mujeledi wake na jiwe. Alimupiga yule Mufilistini na kumwua. Daudi hakukuwa na upanga wowote katika mukono wake.