1 Samweli 13:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
16 Saulo na mwana wake Yonatani pamoja na watu waliokuwa pamoja nao, walikaa kule Gibea katika inchi ya Benjamina na Wafilistini walipiga kambi kule Mikimasi.
Saulo aliwachagua Waisraeli elfu tatu. Kati yao, elfu mbili alikuwa nao kule Mikimasi na katika inchi ya milima ya Beteli. Elfu moja aliwaweka kule Gibea katika eneo la Benjamina. Hao aliwaweka chini ya uongozi wa mwana wake Yonatani. Watu wengine wote waliobakia, aliwarudisha, kila mutu kwake.
Yonatani alishinda kambi ya waaskari ya Wafilistini kule Geba, na Wafilistini wote walisikia juu ya habari hiyo. Hivyo Saulo alipiga baragumu katika inchi yote, akatangaza, akisema: “Waebrania wasikie.”