10 Mara tu alipokuwa anamaliza kutoa sadaka ya kuteketezwa, Samweli akafika. Saulo akatoka inje kwenda kumupokea Samweli na kumusalimia.
Naye anayepita karibu asiwaambie: “Yawe awabariki! Tunawabariki kwa jina la Yawe!”
Nyuma ya muda, Boazi akafika kutoka Betelehemu, akawasalimia wavunaji, akasema: “Yawe akuwe nanyi.” Nao wakamujibu: “Yawe akubariki.”
Samweli alipomufikia Saulo, Saulo akamwambia Samweli: “Yawe akubariki! Nimetimiza amri ya Yawe.”
Kijana mumoja wa Nabali, akamwambia Abigaili, muke wa Nabali: “Daudi alituma wajumbe toka katika jangwa kuja kumusalimia bwana wetu. Lakini yeye aliwatukana.