6 Samweli akawaambia: “Yawe ndiye aliyemuchagua Musa na Haruni na kuwaondoa babu zenu katika inchi ya Misri.
Kisha akamutuma Musa mutumishi wake, akamutuma pamoja na Haruni muchaguliwa wake.
Alipasua jiwe maji yakabubujika; yakatiririka katika jangwa kama muto.
Musa na Haruni walikuwa makuhani wake; Samweli alikuwa kati ya waliomulilia. Walimulilia Yawe naye akawasikiliza.
Haruni na Musa ndio walioambiwa na Yawe: “Mutoe watu wa Israeli kutoka inchi ya Misri, vikundi kwa vikundi.”
Ndio haohao Musa na Haruni walioongea na mufalme wa Misri, juu ya kuwatoa Waisraeli kutoka inchi ya Misri.
Yakobo alikimbilia katika inchi ya Aramu. Akiwa huko alifanya kazi kusudi apate mwanamuke, akachunga kondoo kusudi apate mwanamuke.
Mimi niliwatoa katika inchi ya Misri, niliwakomboa kutoka katika utumwa, niliwapatia Musa, Haruni na Miriamu kwa kuwaongoza.