Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Samweli 12:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Niko hapa, na kama nimefanya tendo lolote baya, basi, mutoe ushuhuda mbele ya Yawe na mbele ya mufalme wake muchaguliwa. Nimenyanganya ngombe dume au punda wa mutu yeyote? Nimemugandamiza mutu yeyote? Nimemutesa mutu yeyote? Nimepokea kituliro kwa mutu yeyote kusudi nifunge macho mbele ya matendo yake? Museme nami nitamurudishia kitu chochote kile.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Samweli 12:3
29 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Maana nimefuata njia za Yawe, wala sikujitenga na Mungu wangu kwa ajili ya uovu.


Leo hii muwarudishie mashamba yao, mashamba yao ya mizabibu, mashamba ya mizeituni na nyumba zao, hata na faida ya feza, ngano, divai, na mafuta ambayo mulikuwa munawalipisha.”


Usitamani nyumba ya mwenzako, wala muke wake, wala mutumwa wake au mujakazi wake, wala ngombe wake, wala punda wake, wala kitu chochote mwenzako anachokuwa nacho.


Mutu akiwakulishia nyama wake katika shamba la mizabibu au kumwachilia nyama wake kula katika shamba la mutu mwingine, atalipa hasara ile kwa mazao bora ya shamba lake mwenyewe au shamba lake la mizabibu.


Usipokee kituliro, maana kituliro kinapofusha wakubwa na kupotosha mambo ya wenye haki.


Anayetamani faida ya unyanganyi anataabisha jamaa yake, lakini anayechukia kituliro ataishi.


Halafu kisha kubadilisha nguo zake atapeleka yale majivu inje ya kambi pahali panapokuwa safi.


Moto wa mazabahu lazima uendelee kuwaka wala usizimike. Kila siku asubui kuhani ataweka kuni kwenye moto huo na juu yake atapanga sadaka ya kuteketezwa, mbele ya kuteketeza mafuta ya sadaka ya amani.


Musa akakasirika sana, akamwambia Yawe: Usikubali sadaka za watu hawa. Mimi sijatwaa punda wa mutu yeyote, wala sijamuzuru mutu!


Wakamujibu: “Ni vya Mufalme wa Roma.” Halafu Yesu akawaambia: “Basi mumupe Mufalme wa Roma vinavyokuwa vyake, na Mungu vinavyokuwa vyake.”


Lakini Zakayo akasimama mbele ya Bwana na kumwambia: “Bwana! Ninawapa masikini nusu ya mali zangu, na kama nimetwaa kitu cha mutu kwa kumudanganya, nitamurudishia mara ine sawa na kitu kile.”


Mimi sikutamani feza, zahabu, wala nguo ya mutu yeyote.


Sasa mimi niko tayari kufika kwenu kwa mara ya tatu, nami sitawalemea. Maana sihitaji mali yenu, lakini ninawahitaji ninyi. Kwa sababu si kazi ya watoto kuwawekea wazazi wao akiba, lakini ni kazi ya wazazi kuwawekea watoto wao akiba.


Musipotoshe haki, musikuwe na upendeleo, wala musikubali kupokea kituliro, kwa kuwa kituliro kinapofusha macho ya watu wenye hekima na kupotosha maneno ya mutu mwenye haki.


Ninyi ni washuhuda wetu, na Mungu vilevile anashuhudia kwamba tulipokaa kati yenu ninyi waamini, tuliishi katika utakatifu na haki, na bila kosa.


Kama vile munavyojua, hata siku moja hatukutumia masemi ya kujipendekeza kwa watu wala hatukutamani kupata mali kwa uficho; Mungu ni mushuhuda wetu.


Ninawaonya, muchunge lile kundi Mungu alilowapatia, si kwa kulazimishwa, lakini kwa mapenzi yenu sawa vile Mungu anavyotaka. Musitumike kwa ajili ya tamaa mbaya ya mali, lakini kwa kujitoa kwa moyo mwema.


Halafu Samweli akatwaa chupa ndogo ya mafuta akamumiminia Saulo juu ya kichwa, akamubusu na kumwambia: “Yawe amekutia mafuta ukuwe mutawala juu ya watu wake.


Watu wakamujibu: “Haujatudanganya hata kidogo, haujatugandamiza, wala haujakamata kitu chochote kwa mutu.”


Samweli akajibu: “Yawe ni mushuhuda juu yenu, na mufalme wake muchaguliwa leo ni mushuhuda kuwa mumeniona sina kosa.” Wao wakajibu: “Yeye ni mushuhuda.”


Kisha, nitajiinulia kuhani mwingine mwaminifu atakayefanya kulingana na yale yanayokuwa ndani ya moyo na akili yangu. Nitamujengea ukoo imara, naye atatumika siku zote mbele ya mufalme wangu muchaguliwa.


Sasa, leo umejionea kwa macho yako mwenyewe. Ulipokuwa ndani ya pango Yawe alikutia katika mikono yangu. Wamoja kati ya watu wangu waliniambia nikuue, lakini nilikuhurumia. Nikasema sitanyoosha mukono wangu juu ya bwana wangu maana yeye ni muchaguliwa wa Yawe.


Daudi akaanza kufazaika ndani ya moyo kwa sababu alikata pindo la nguo ya Saulo kwa siri.


Akawaambia watu wake: “Yawe anizuie nisimutendee kitendo kama hiki bwana wangu ambaye ni muchaguliwa wa Yawe. Nisiunyooshe mukono wangu juu ya mutu ambaye Yawe amemupakaa mafuta.”


Lakini Yawe anakataza nisinyooshe mukono wangu juu ya mutu ambaye ni muchaguliwa wa Yawe. Lakini twaa mukuki wake unaokuwa karibu na kichwa chake pamoja na mufuko wake wenye maji, halafu tujiendee zetu.”


Lakini Daudi akamwambia Abisai: “Usimwangamize; maana nani anaweza kunyoosha mukono wake juu ya mutu ambaye ni muchaguliwa wa Yawe, naye asiazibiwe?


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ