“Yawe atawapeleka ninyi na mufalme wenu mutakayejichagulia, mpaka kwa taifa ambalo ninyi hamukulijua wala wazee wenu. Na huko mutatumikia miungu mingine ya miti na mawe.
Kama mukivunja agano la Yawe, Mungu wenu, ambalo aliwaamuru mulishike, mukienda kuitumikia miungu mingine na kuinama mbele yao; basi, hasira ya Yawe itawaka juu yenu, nanyi mutaangamia mara moja kutoka inchi hii nzuri ambayo amewapa.”