Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Samweli 12:21 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

21 Musiifuate miungu ya uongo isiyokuwa na faida wala haiwezi kuwaokoa, maana ni ya uongo.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Samweli 12:21
21 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Walikataa kutii masharti yake; hawakushika agano alilofanya na babu zao, walizarau maonyo yake, waliabudu sanamu zisizokuwa na maana hata wao wenyewe hawakukuwa na maana tena, walifuata desturi za mataifa yaliyowazunguka: walizarau amri za Yawe; wala hawakuzishika.


Miungu hiyo yote ni udanganyifu, haiwezi kufanya kitu chochote; sanamu zao ni upepo tu, hazina maana.


Enyi watu wa mataifa muliobaki, mukusanyike pamoja mukuje! Ninyi mumekosa akili: ninyi munabeba sanamu za miti na kumwomba mungu asiyeweza kuokoa watu.


Wanajibebesha sanamu hiyo juu ya mabega na kuipeleka, kisha wanaiweka pahali pake, nayo inakaa palepale; haiwezi hata kidogo kusogea kutoka pale inapokuwa. Mutu akiililia, haiwezi kumwitikia, wala haiwezi kumwokoa mutu katika taabu zake.


Hazina faida, ni udanganyifu mutupu; wakati zitakapoazibiwa zote zitaangamia.


Wote ni wajinga na wapumbafu, fundisho la sanamu hizi ni mazarau matupu!


Katikati ya miungu ya uongo ya mataifa nani anayeweza kunyesha mvua? Au, ni mbingu ndiyo inaweza kutoa manyunyu? Si ni wewe ee Yawe, Mungu wetu? Tunakuwekea wewe tumaini letu, maana ni wewe unayefanya haya yote.


Ee Yawe! Wewe ndiwe nguvu yangu na upango wangu; wewe ni kimbilio langu wakati wa taabu. Mataifa toka pande zote za dunia yatakufikia na kusema: Miungu ya babu zetu ilikuwa ya uongo, ilikuwa ya bure, isiyofaa kitu.


Watu wangu wametenda maovu mawili; wameniacha mimi ninayekuwa chemichemi ya maji ya uzima, wakajichimbia visima vyao wenyewe, visima vyenye nyufa, visivyoweza kuchunga maji.


Yawe anasema hivi: Babu zenu waliona kosa gani kwangu hata wakanigeuka na kuniacha, wakakimbilia miungu ya bure, hata nao wakakuwa watu bure?


Roho yangu ilipoanza kunitoka, nilikukumbuka, ee Yawe, maombi yangu yakakufikia katika hekalu lako takatifu.


Watu wanaoabudu sanamu za miungu ya bure, wanautupilia mbali uaminifu wao kwako.


Sanamu mutu aliyotengeneza inafaa kwa nini? Sanamu ni madini yaliyoyeyushwa, ni kitu cha kueneza udanganyifu! Mutengenezaji wa sanamu anatumainia kile alichotengeneza mwenyewe, sanamu ambayo haiwezi hata kusema!


“Wandugu, kwa sababu gani munafanya mambo kama haya? Sisi vilevile ni watu, tuko sawasawa nanyi, na tunawahubiri ninyi Habari Njema kwamba muache kuabudu vitu hivi vya bure na mumugeukie Mungu mwenye uzima; yeye aliyeumba mbingu na dunia, bahari na vyote vinavyokuwa ndani yao.


Basi kuelekea lile ulizo juu ya kula nyama za kutambikiwa kwa sanamu za miungu, tunajua kwamba sanamu ni kitu bure katika dunia, na ya kuwa kuna Mungu mumoja peke yake tu.


Mufanye angalisho kusudi mioyo yenu isidanganywe, mukigeuka na kutumikia miungu mingine na kuiabudu,


Lakini mukipotoshwa na kukataa kumusikiliza, mukivutwa kuabudu miungu mingine na kuitumikia,


Wamenichochea kuona wivu kwa kitu kisichokuwa mungu, wamenikasirikisha kwa sanamu zao. Hivyo nitawafanya waone wivu juu ya watu wa bure, nitawakasirikisha kwa kutumia taifa la wapumbafu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ