Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Samweli 12:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Sasa, munakuwa na mufalme wa kuwaongoza. Kwa upande wangu, mimi ni muzee mwenye imvi, na wana wangu wako pamoja nanyi. Nimekuwa kiongozi wenu tangu nilipokuwa kijana mpaka sasa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Samweli 12:2
17 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Usiniachilie, ee Mungu, nitakapokuwa muzee mwenye imvi nyingi, kusudi nivitangazie vizazi vitakavyokuja nguvu yako.


ambaye atawatangulia na kuwaongoza katika shuguli zao zote, kusudi wasikuwe kama kondoo wasiokuwa na muchungaji.


Kwa maana, mimi sasa niko tayari kutolewa kama sadaka, na wakati wa kufa kwangu umekaribia.


Nyuma ya muda murefu, Yawe aliwajalia Waisraeli amani kwa kuwaokoa na waadui zao pande zote. Wakati ule Yoshua alikuwa muzee wa miaka mingi.


Yoshua aliwaita Waisraeli wote pamoja na viongozi na wazee wao, waamuzi na wakubwa, akawaambia: “Sasa mimi nimekuwa muzee wa miaka mingi.


Kwa maana ninajua kwamba ninakaribia kuacha mwili huu unaokuwa wa kufa kama vile Bwana wetu Yesu Kristo alivyonionyesha waziwazi.


Wakati ule, Eli alikuwa muzee sana. Aliposikia yote ambayo wana wake walikuwa wanawatendea Waisraeli, jinsi walivyokuwa wanalala na wanawake waliokuwa wanatumika kwenye mulango wa Hema ya Kusanyiko,


Kwa nini basi, umezionea wivu matoleo na sadaka nilizowaamuru watu waniletee, nawe ukawaheshimu watoto wako kuliko mimi kwa kujinenepesha wenyewe kwa kula sehemu nzuri za sadaka ambazo watu wangu wa Israeli wananitolea?


Kisha Yawe akakuja na kusimama hapo, akamwita Samweli kama pale mbele: “Samweli! Samweli!” Samweli akasema: “Sema, maana mimi mutumishi wako ninasikiliza.”


Nimekwisha kumwambia kwamba nitaiazibu jamaa yake milele, kwa uovu anaoujua kwa sababu wana wake wamenikufuru mimi na hakuwazuia.


Hata hivyo, Eli alimwita Samweli, akamwambia: “Mwana wangu Samweli.” Samweli akaitika: “Niko hapa!”


Samweli alipokuwa muzee, aliwafanya wana wake kuwa waamuzi wa Waisraeli.


kusudi nasi vilevile tukuwe sawa mataifa mengine. Mufalme wetu, atatuamulia haki zetu, atatuongoza na kutupigania vita vyetu.”


Lakini watoto hao hawakufuata mwenendo wa baba yao. Lakini walianza kujitafutia faida. Wakapokea kituliro na kupotosha haki.


wakamwambia: “Angalia, wewe sasa ni muzee na watoto wako hawafuati mwenendo wako. Hivyo, utuchagulie mufalme wa kututawala sawa vile inavyokuwa kwa mataifa mengine.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ