16 Kwa hiyo basi, mutulie na kulitazama jambo hilo kubwa ambalo Yawe atatenda mbele yenu.
Musa akawaambia Waisraeli: “Musiogope! Musimame imara! Leo mutaona jinsi Yawe atakavyowaokoa. Maana, hawa Wamisri munaowaona leo, hamutawaona tena.
Waisraeli walipoona tendo hilo la ajabu Yawe alilofanya mbele ya Wamisri, wakamwogopa. Wakamwamini Yawe na Musa mutumishi wake.
Sasa musimame palepale munapokuwa kusudi mimi na ninyi tuhukumiwe mbele ya Yawe, nami nitawahutubia juu ya matendo yake ya ajabu ambayo aliyatenda kwa kuwaokoa ninyi na babu zenu.
Samweli akamwambia Saulo: “Nyamaza! Nitakuambia jambo Yawe aliloniambia leo usiku.” Saulo akasema: “Uniambie.”