naye akatoka kwenda kukutana na mufalme Asa, akamwambia: “Unisikilize, ee Asa na watu wote wa kabila la Yuda na la Benjamina! Yawe yuko pamoja nanyi, ikiwa mutakuwa pamoja naye. Mukimutafuta, mutamupata, lakini mukimwacha, naye atawaacha.
Lakini Yawe amefanya sawa kwa maana nimeliasi neno lake. Munisikilize enyi watu wote, muyaangalie mateso yangu. Wabinti zangu na vijana wangu wanaume wamepelekwa katika utumwa.
Kila mara walipokwenda kupigana, mukono wa Yawe ulipambana nao kwa kuwaletea hasara, kama alivyokuwa amewaonya na kuapa. Nao wakakuwa katika huzuni kubwa.
Lakini wao walimusahau Yawe, Mungu wao, naye akawatia katika mikono ya Sisera, jemadari wa waaskari wa muji wa Hazori, na katika mikono ya Wafilistini na katika mikono ya mufalme wa Moabu. Mataifa hayo yalipigana na babu zenu na kuwashinda.
Lakini kisha kulipeleka kule Gati, Yawe akauazibu muji huo, akitia hofu kubwa katika muji, na akawapiga wanaume wa muji huo, vijana kama vile wazee, kwa kuwaletea majipu.