Samweli akawaambia watu wote: “Huyu ndiye mutu aliyechaguliwa na Yawe kati ya watu wote; hakuna yeyote anayekuwa kama yeye.” Watu wote wakapiga kelele: “Mufalme aishi milele.”
Watu wote wakaenda Gilgali, na walipofika kule, wakamusimika Saulo kuwa mufalme mbele ya Yawe. Wakamutolea Yawe sadaka za amani pale. Na Saulo pamoja na watu wote wa Israeli wakafurahi sana.
Sasa si wakati wa kuvuna ngano? Lakini mimi nitamwomba Yawe alete radi na mvua, nanyi mutatambua na kuona kwamba uovu wenu muliotenda mbele ya Yawe kwa kujitakia mufalme, ni mukubwa.”
Hivyo wakamwambia Samweli: “Tafazali, utuombee sisi watumishi wako kwa Yawe, Mungu wako, kusudi tusikufe; kwa sababu tumezidisha zambi zetu kwa uovu huo wa kujitakia mufalme.”
wakamwambia: “Angalia, wewe sasa ni muzee na watoto wako hawafuati mwenendo wako. Hivyo, utuchagulie mufalme wa kututawala sawa vile inavyokuwa kwa mataifa mengine.”
Na juu ya wale punda waliopotea siku tatu zilizopita, musikuwe na wasiwasi juu yao; wamekwisha kupatikana. Lakini ni nani yule ambaye Waisraeli wanamutaka sana? Si wewe na jamaa yote ya baba yako?”