Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Samweli 12:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Halafu Yawe alimutuma Yerubali, na kisha akamutuma Bedani, kisha Yefuta, na kwa mwisho akanituma mimi Samweli. Kila mumoja wetu aliwaokoa kutoka waadui zenu waliowazunguka, nanyi mukaishi kwa amani.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Samweli 12:11
13 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yawe akawapa Waisraeli kiongozi ambaye aliwakomboa kutoka kwa Waaramu. Halafu wakakaa kwa amani kama vile walivyokuwa zamani.


Rakemu alizaa Bedani. Hawa wote ni wazao wa Gileadi, mwana wa Makiri, mujukuu wa Manase.


Siku moja akamwita Baraka mwana wa Abinoamu wa Kedesi katika inchi ya Nafutali. Alipokuja akamwambia: “Yawe, Mungu wa Israeli, anakuamuru hivi: ‘Kwenda ukusanye watu wako kwenye mulima Tabori, uchague watu elfu kumi kutoka makabila ya Nafutali na Zebuluni.


Yawe akamugeukia, akamwambia: “Kwenda kwa uwezo unaokuwa nao, uikomboe Israeli kutoka Wamidiani. Ni mimi ninayekutuma.”


Yoasi akawaambia wale wote waliomufuata: “Muko munamutetea Bali? Ninyi, mutamwokoa? Yeyote atakayemutetea atauawa mbele ya mapambazuko. Kama Bali ni mungu, basi, ajitetee mwenyewe maana mazabahu yake imebomolewa.”


Siku hiyo wakamwita Gideoni “Yerubali” maana yake “Bali ajitetee”, maana aliibomoa mazabahu ya mungu Bali.


Yerubali, ni kusema Gideoni na watu wote waliokuwa pamoja naye wakaamuka mapema, wakapiga kambi yao katika bonde karibu na chemichemi ya Harodi. Kambi ya Wamidiani ilikuwa upande wao wa kaskazini katika bonde karibu na mulima More.


Gideoni, ni kusema Yerubali mwana wa Yoasi, akarudi kwake na kukaa kule.


Tena, hawakuitendea mema jamaa ya Yerubali, ni kusema Gideoni kwa mema yote aliyoyatenda katika Israeli.


Watu wote katika inchi ya Israeli toka Dani, upande wa kaskazini, mpaka Beri-Seba, upande wa kusini, wakajua kwamba Samweli alikuwa nabii mwaminifu wa Yawe.


Siku hiyo Wafilistini walishindwa na Yawe aliwazuia Wafilistini kuishambulia inchi ya Israeli wakati wote Samweli alipokuwa anaishi.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ