Halafu Yoabu alimupelekea mufalme jumla ya watu. Katika inchi ya Israeli kulikuwa wanaume mashujaa elfu mia ine wenye ujuzi wa kutumia mapanga; na katika Yuda, kulikuwa wanaume elfu mia tano.
Viongozi wote wa makabila ya Israeli wakajitokeza mbele ya mukusanyiko wa watu wa Mungu. Wote kwa jumla walikuwa waaskari elfu mia ine wa miguu wenye silaha.
Wakawaambia wale wajumbe waliorudi kutoka Yabesi: “Muwaambie wakaaji wa Yabesi-Gileadi hivi: kesho, wakati jua linapokuwa kali, mutakuwa mumekombolewa.” Watu wa Yabesi walipopata habari hizo walifurahi sana.
Samweli akaondoka kutoka Gilgali na kwenda kule Gibea katika inchi ya Benjamina. Saulo alipowahesabu watu waliokuwa pamoja naye, akaona wako watu mia sita tu.
Saulo akaita waaskari wake, akawahesabu kule Telaimu. Kulikuwa waaskari wa miguu elfu mia mbili kutoka katika inchi ya Israeli na elfu kumi kutoka inchi ya Yuda.