Kutoka pale utakwenda kwenye muti wa mwalo wa Tabori, pahali ambapo utakutana na wanaume watatu wakiwa katika njia kwenda kumutolea Mungu sadaka, kule Beteli. Mumoja wao atakuwa akipeleka wana-mbuzi watatu, wa pili atakuwa akipeleka mikate mitatu na wa tatu atakuwa akibeba karabia ya divai.
Kisha, utafika kule Gibeati-Elohimu, pahali ambapo pana kambi ya waaskari wa Wafilistini. Pale, utakapokuwa unakaribia muji, utakutana na kundi la manabii. Manabii hao watakuwa wanatoka kwenye nafasi ya kuabudia na wakipiga vinubi, matari, filimbi na zeze, na watakuwa wanatabiri.