Basi, utupatie watu saba kati ya wazao wake, nasi tuwatundike mbele ya Yawe juu ya mulima Gibea, kwa Saulo aliyechaguliwa na Yawe.” Mufalme akasema: “Nitawapatia nao.”
Basi, viongozi wa ukoo za makabila ya Yuda na Benjamina wakaondoka, makuhani na Walawi, na kila mutu ambaye Mungu alimupa moyo wa kwenda kujenga upya nyumba ya Yawe, inayokuwa Yerusalema.
Wakati watu wa mataifa mengine waliposikia maneno haya wakafurahi, wakatukuza neno la Bwana. Nao wote waliokuwa wamechaguliwa kwa kupata uzima wa milele, wakaamini.
akamwokoa toka katika taabu yote aliyopata. Mungu akamujalia neema, apate kupendwa na Mufalme wa Misri na kuonekana kuwa mwenye hekima mbele yake. Mufalme yule akamuweka kuwa musimamizi wa inchi yake na wa nyumba yake yote.
Saulo aliwachagua Waisraeli elfu tatu. Kati yao, elfu mbili alikuwa nao kule Mikimasi na katika inchi ya milima ya Beteli. Elfu moja aliwaweka kule Gibea katika eneo la Benjamina. Hao aliwaweka chini ya uongozi wa mwana wake Yonatani. Watu wengine wote waliobakia, aliwarudisha, kila mutu kwake.