Alimufukuza inje. Akaweka makerubi upande wa mashariki wa bustani ya Edeni wakiwa na upanga wa moto uliogeuka huku na kule, kwa kulinda njia inayokwenda kwenye muti wa uzima.
Lakini Yawe alimwambia: “Usiangalie sura yake wala urefu wake. Mimi nimemukataa maana siangalii mambo kama vile wanadamu wenye kufa wanavyoangalia. Mwanadamu anaangalia umbo la inje, lakini mimi ninaangalia ndani ya moyo.”
Katika kabila la Benjamina, kulikuwa mutu mumoja tajiri aliyeitwa Kisi. Yeye alikuwa mwana wa Abieli, mujukuu wa Zerori, wa jamaa ya Bekorati mwana wa Afia wa kabila la Benjamina.
Kisi alikuwa na mwana aliyeitwa Saulo. Saulo alikuwa kijana mwenye sura nzuri, na hakuna mutu katika Israeli aliyelingana na Saulo kwa uzuri. Saulo alikuwa murefu zaidi kuliko mutu yeyote katika inchi ya Israeli; watu wote walimufikia kwenye mabega.