Mimba hiyo ilikuwa ya mapacha. Watoto hao waligongana ndani ya tumbo la Rebeka, naye akasema: “Kama hivi ndivyo mambo yanavyokuwa, kwa nini kuishi?” Basi, akakwenda kumwuliza Yawe.
Nyuma ya mambo yale, Daudi alimwomba Yawe shauri, akasema: “Niende kwenye muji mumoja kati ya miji ya Yuda?” Yawe akamwambia: “Kwenda!” Daudi akamwuliza: “Niende katika muji gani?” Yawe akamujibu: “Kwenda kwenye muji wa Hebroni.”
Wakati mumoja katika siku za utawala wa Daudi kukatokea njaa kali katika inchi. Njaa hiyo ilidumu miaka mitatu yenye kufuatana. Daudi alimwomba Yawe shauri. Yawe akamwambia: “Saulo na jamaa yake wana makosa ya kumwanga damu kwa sababu aliwaua Wagibeoni.”
Yeye atamutegemea kuhani Eleazari ambaye atamujulisha mapenzi yangu kwa kutumia jiwe la shauri. Kwa njia hii, Eleazari atamwongoza Yoshua na Waisraeli wote wanapotoka na wanapoingia.
Waisraeli wakaenda Beteli kuomba shauri kwa Mungu, wapate kujua kabila ambalo litakwenda kwanza kupigana na watu wa kabila la Benjamina. Yawe akataja kabila la Yuda liende kwanza.
Basi Waisraeli wakaenda juu, wakamulilia Yawe mpaka magaribi. Kisha wakaomba shauri kwa Yawe: “Twende tena kupigana na wandugu zetu, wa kabila la Benjamina?” Yawe akawajibu: “Muende mupigane nao.”
Finehasi mwana wa Eleazari mwana wa Haruni alikuwa na kazi ya kutumika mbele yake. Waisraeli wakamwuliza Yawe: “Twende tena kupigana na wandugu zetu, watu wa kabila la Benjamina?” Yawe akawaambia: “Muende. Kesho nitawatia katika mikono yenu.”
Akalileta mbele kabila la Benjamina, kulingana na ukoo zake, na ukoo wa Matiri ukachaguliwa kwa kura. Mwisho akauleta mbele ukoo wa Matiri, na Saulo mwana wa Kisi akachaguliwa kwa kura. Lakini walipomutafuta hakupatikana.
Samweli akamwambia: “Ingawa unajiona kwamba wewe ni mudogo, lakini si wewe kiongozi wa makabila ya Israeli? Yawe alikupakaa mafuta kwa kukusimika kuwa mufalme juu ya Israeli.
Saulo akajibu: “Mimi ni wa kabila la Benjamina, kabila dogo kuliko makabila yote ya Waisraeli. Na katika kabila lote la Benjamina jamaa yangu ndiyo ndogo kabisa. Lakini, kwa nini unanizungumuzia namna hiyo?”