13 Saulo alipomaliza kutabiri, alikwenda kwenye nafasi ya kuabudia.
Mutu fulani, mukaaji wa pahali pale, akasema: “Baba yao ni nani?” Hivyo kukatokea mezali inayosema: “Hata Saulo ni mumoja wa manabii?”
Baba mudogo wa Saulo alipowaona Saulo na mutumishi, akawauliza: “Mulikuwa wapi?” Saulo akajibu: “Tulikwenda kuwatafuta punda, na tulipoona hawapatikani, tulikwenda kumwona Samweli.”