Walipotambua kwamba yeye ndiye yule kiwete aliyekuwa akiikaa na kuombaomba musaada kwenye mulango wa hekalu unaoitwa “Muzuri,” wakashikwa na hofu na kushangaa sana na mambo yale yaliyomutokea.
Wajumbe wa Baraza Kubwa walishangaa sana kuona namna Petro na Yoane walivyosema bila woga na kujua kwamba walikuwa watu wasiojulikana na wasiokuwa na elimu. Wakatambua kwamba walikuwa pamoja na Yesu.
Wote waliomusikia walishangaa, wakisema: “Si mutu huyu ndiye aliyewatesa vikali kule Yerusalema watu wanaoomba kwa jina la Yesu? Hakika amefika huku nako kusudi awafunge watu kama hao na kuwapeleka kwa wakubwa wa makuhani.”
Alivua nguo zake, akatabiri mbele ya Samweli. Alibaki uchi kwa siku moja, muchana na usiku. Kwa hiyo watu walianza kujiuliza: “Hata Saulo ni mumoja wa manabii?”