Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Samweli 1:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Elekana alimupa Hana fungu kubwa la nyama ya sadaka kwa sababu alimupenda sana ingawa Yawe hakumujalia watoto.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Samweli 1:5
9 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Sarai hakukuwa na mutoto kwa sababu alikuwa tasa.


Basi, Sarai, muke wa Abramu, alikuwa bado hajamuzalia mutoto, naye alikuwa na mujakazi aliyeitwa Hagari, kutoka Misri.


Hapo mbele Yawe alikuwa amewazuia wanawake wote wa nyumba ya Abimeleki kupata watoto kwa sababu ya Sara, muke wa Abrahamu.


Rakeli alipoona kwamba hajamuzalia Yakobo watoto, alimwonea Lea dada yake wivu, akamwambia Yakobo: “Unipatie watoto, kama sivyo, nitakufa.”


Yakobo akamukasirikia Rakeli na kumwambia: “Mimi nimekuwa pahali pa Mungu aliyekuzuia kupata watoto?”


Chakula kilikuwa kikitwaliwa kutoka kwenye meza ya Yosefu na kupelekwa kwao, lakini Benjamina alipewa mara tano zaidi ya kipimo wandugu zake walichopewa. Basi, wakakunywa na kufurahi pamoja naye.


Aliwapa kila mumoja wao nguo za kubadilisha, lakini akamupa Benjamina vikoroti mia tatu vya feza na nguo tano za kubadilisha.


“Ikiwa mwanaume fulani ana wake wawili naye anamupenda mumoja kuliko mwingine, nao wanawake hao wamemuzalia watoto wanaume, na mutoto wa kwanza kuzaliwa ni wa yule mama asiyemupenda,


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ