4 Kila wakati Elekana alipotoa sadaka alimupa muke wake Penina fungu moja la nyama ya sadaka na fungu mojamoja kwa watoto wake wa kiume na wa kike.
Atatoa vilevile zile figo mbili na mafuta yake pamoja na ile sehemu bora ya maini.
Nyama ya sadaka hiyo ya amani ya kumushukuru Mungu itakuliwa siku hiyohiyo inapotolewa. Hataacha hata sehemu yake mpaka asubui.
Mutafurahia mbele ya Yawe, Mungu wenu, ninyi pamoja na wana wenu na wabinti zenu, watumishi wenu, Walawi, wageni, wayatima na wajane ambao wanaishi pamoja nanyi. Mufanye haya katika pahali Yawe, Mungu wenu, atakapochagua kwa ajili ya jina lake.