Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Samweli 1:28 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

28 Kwa sababu hiyo, mimi ninamupa Yawe mutoto huyu; wakati wote atakapokuwa anaishi, ametolewa kwa Yawe.” Halafu, wakamwabudu Yawe pale.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Samweli 1:28
12 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Halafu yule mutu akainamisha kichwa chake, akamwabudu Yawe


Kisha nikainama na kumwabudu Yawe. Nikamutukuza Yawe, Mungu wa bwana wangu Abrahamu, ambaye ameniongoza moja kwa moja kwa binti wa ukoo wa bwana wangu kwa ajili ya mwana wake.


Mutumishi wa Abrahamu aliposikia maneno hayo, akamwabudu Yawe.


Nikuambie nini mwana wangu? Nikuambie nini mwana wangu niliyezaa? Nikuambie nini wewe niliyeomba kwa Mungu?


Muda wote atakaokuwa munaziri atakuwa mutakatifu kwa Yawe.


Tena, tangia utoto wako unajua Maandiko Matakatifu yanayoweza kukupatia hekima kusudi uokolewe kwa njia ya kumwamini Kristo Yesu.


Gideoni aliposikia masimulizi hayo ya ndoto na mafasirio yake, akamwabudu Mungu. Kisha akarudi kwenye kambi ya Waisraeli, akasema: “Musimame tuende, maana Yawe amelitia jeshi la Wamidiani katika mikono yenu.”


Akafanya kiapo akisema: “Ee Yawe wa majeshi, kama tu utayaangalia mateso yangu mimi mujakazi wako, ukinikumbuka mimi, bila kunisahau, mimi mujakazi wako, ukinijalia mimi mujakazi wako mutoto mwanaume, nitakupa wewe Yawe mutoto huyo akuwe wako maisha yake yote; wembe hautapita kwenye kichwa chake hata kidogo.”


Lakini mara hii Hana hakuenda, maana alimwambia mume wake hivi: “Mara tu mutoto atakapoachishwa kunyonya, nitamupeleka kusudi awekwe mbele ya Yawe, abakie kule siku zote.”


Kisha, Elekana akarudi kwake Rama. Lakini mutoto Samweli akabaki Shilo kwa kumutumikia Yawe chini ya uongozi wa kuhani Eli.


Eli aliwabariki Elekana na muke wake, akisema: “Yawe akupe wewe Elekana watoto wengine kwa mwanamuke huyu kusudi wakamate nafasi ya yule uliyemupa Yawe.” Kisha wao walirudi kwao.


Daudi akamujibu Akisi: “Kweli! Utaona kitu ambacho mutumishi wako anaweza kufanya.” Akisi akamwambia: “Nami nitakufanya kuwa mulinzi wangu wa pekee wa maisha.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ