Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Samweli 1:19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

19 Kesho yake asubui, Elekana na jamaa yake waliamuka asubui mapema, na kisha kumwabudu Yawe, walirudi kwao Rama. Elekana akalala na muke wake Hana na Yawe akamukumbuka.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Samweli 1:19
23 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yawe akamukumbuka Sara, akamutendea kama alivyoahidi.


Kisha Mungu akamukumbuka Rakeli, akakubali ombi lake na kumujalia kupata watoto.


Adamu akalala na muke wake Eva, naye akapata mimba, akazaa Kaina. Eva akasema: “Nimepata mutoto mwanaume kwa musaada wa Yawe!”


Kisha Mungu akamukumbuka Noa na nyama wote wa pori na wa kufugwa waliokuwa pamoja naye ndani ya chombo. Basi, Mungu akavumisha upepo juu ya inchi, maji yakaanza kupunguka.


Lakini yule mwanamuke akapata mimba na kuzaa mutoto wakati kama ule mwaka uliofuata, kama vile Elisha alivyokuwa amemwambia.


Ninaamuka mbele ya mapambazuko na kukuomba musaada; ninaweka tumaini langu katika maneno yako.


Alitukumbuka wakati wa uzaifu wetu. Wema wake unadumu milele.


Usikumbuke zambi na makosa ya ujana wangu; unikumbuke kwa kadiri ya wema wako, kwa ajili ya uzuri wako, ee Yawe.


Usikilize kilio changu, Mufalme wangu na Mungu wangu, maana wewe ndiwe ninayekuomba.


Lakini mimi ninamulilia Mungu, naye Yawe ataniokoa.


Kesho yake asubui kulipokuwa kungali giza, Yesu akaamuka, akatoka katika muji na kwenda pahali penye ukiwa, kule akaanza kuomba.


Na akaongeza kusema: “Ee Yesu, usinisahau wakati utakapokuja katika ufalme wako!”


Kulikuwa mutu mumoja katika muji wa Rama katika inchi ya milima ya Efuraimu jina lake Elekana wa kabila la Efuraimu. Yeye alikuwa mwana wa Yerohamu, na mujukuu wa Elihu mwana wa Tohu mwana wa Zufu.


Akafanya kiapo akisema: “Ee Yawe wa majeshi, kama tu utayaangalia mateso yangu mimi mujakazi wako, ukinikumbuka mimi, bila kunisahau, mimi mujakazi wako, ukinijalia mimi mujakazi wako mutoto mwanaume, nitakupa wewe Yawe mutoto huyo akuwe wako maisha yake yote; wembe hautapita kwenye kichwa chake hata kidogo.”


Kisha, Samweli akaenda Rama; na mufalme Saulo akarudi kwenye nyumba yake kule Gibea.


Samweli akatwaa pembe lake lenye mafuta akamupakaa Daudi mafuta mbele ya kaka zake. Mara moja roho wa Yawe akamushika Daudi kwa nguvu na kuwa naye tangu siku hiyo. Kisha Samweli akarudi katika muji wa Rama.


Daudi alipotoroka, alikwenda Rama kwa Samweli. Alimwelezea Samweli mambo yote aliyomufanyia Saulo. Basi, Daudi na Samweli walikwenda na kukaa kule Nayoti.


Kisha, Elekana akarudi kwake Rama. Lakini mutoto Samweli akabaki Shilo kwa kumutumikia Yawe chini ya uongozi wa kuhani Eli.


Sasa, Samweli akakufa. Nao Waisraeli wote wakakusanyika kwa kumwomboleza. Wakamuzika kwenye nyumba yake kule Rama. Kisha Daudi akaenda zake kwenye jangwa za Parani.


Kisha, alikuwa akirudi Rama, maana kule ndiko kulikuwa kwake. Aliwaamulia Waisraeli haki zao kule, na kumujengea Yawe mazabahu kule.


Basi, viongozi wote wa Waisraeli walikusanyika pamoja, na kumwendea Samweli katika muji wa Rama,


Kesho yake asubui mapema, Samweli alimwita Saulo kutoka juu ya dari: “Amuka, kusudi nikusindikize urudi kwa nyumba.” Saulo aliamuka, na wote wawili, yeye na Samweli, wakatoka na kwenda katika barabara.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ