1 Petro 4:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 20023 Kufuatana na hiyo, zamani mulipitisha siku nyingi mukifanya matendo yanayolingana na ya wapagani. Mulizoea kuishi katika uasherati, tamaa mbaya, ulevi, karamu za ulafi, za ulevi na kuabudu sanamu. အခန်းကိုကြည့်ပါ။ |
Asa aliposikia maneno haya, ni kusema unabii wa Azaria mwana wa Odedi, yakamutia moyo. Akaondoa sanamu zote za kuchukiza katika inchi yote ya Yuda na ya Benjamina, na kutoka katika miji yote aliyoteka katika inchi ya milima ya Efuraimu. Na kisha akatengeneza upya mazabahu ya Yawe iliyokuwa katika baraza la nyumba ya Yawe.
Maana kuna watu wasiomuheshimu Mungu waliojiingiza kwa siri kati yetu. Watu hawa wanapotosha ujumbe wa neema ya Mungu wetu kusudi wapate kufanya uasherati na kumukana Yesu Kristo, anayekuwa peke yake Kiongozi na Bwana wetu. Tangia zamani Maandiko Matakatifu yamejulisha hukumu ile itakayowapata watu hawa.