Ngamia walipotosheka kunywa maji, yule mutu akamupa yule binti pete ya zahabu yenye uzito wa yapata grama sita, na vikomo viwili vya zahabu za grama kumi kila moja.
Halafu nilimwuliza: ‘Wewe ni binti ya nani?’ Akaniambia: ‘Mimi ni binti ya Betueli mwana wa Milka, muke wa Nahori.’ Halafu nikamupa pete na kumuvalisha vikomo kwa mikono.
Yehu alipofika Yezereheli, Yezebeli alikuwa amekwisha kupata habari ya mambo yaliyotokea. Alijipakaa rangi kwenye macho na kuchanua nywele zake, kisha akaenda kwenye dirisha na kuangalia chini.
Kisha siku tatu ya kufunga kwake, Esteri akavaa nguo zake za kimalkia, akaenda kusimama katika kiwanja cha ndani cha nyumba ya mufalme, kuelekea chumba cha mufalme. Mufalme alikuwa mule ndani akiikaa katika kiti chake cha kifalme, kuelekea mulango wa nyumba ya mufalme.
Kila mwanamuke Mwebrania atamwomba jirani yake Mumisri, au mugeni wake anayekuwa katika nyumba yake, amupe vyombo vya feza na zahabu pamoja na nguo. Hivyo mutawavalisha watoto wenu wanaume na wanawake. Ndivyo mutakavyowanyanganya Wamisri mali yao.”
Hivyo wote wenye moyo safi, wanaume na wanawake, wakaleta pete za masikio na za muhuri, vikuku na kila aina ya mapambo ya zahabu. Kila mutu akamutolea Yawe kitu cha zahabu.
Kisha akatengeneza birika la shaba na tako lake la shaba. Birika hilo lilitengenezwa kwa kutumia vioo vya shaba vya wanawake waliotumika kwenye mulango wa hema la mukutano.
Amuka! Amuka! Ujipatie zile nguvu zako, ewe Sayuni! Uvae nguo yako nzuri, ewe Yerusalema, muji mutakatifu. Maana hawataingia tena kwako watu wasiotahiriwa na wachafu.
Nitafurahi sana kwa sababu ya Yawe, nafsi yangu itashangilia kwa sababu ya Mungu wangu. Maana amenivalisha nguo ya wokovu, amenifunika kanzu ya haki, kama bwana arusi anavyojipamba kwa shada la maua, kama bibi arusi anavyojipamba kwa ushanga wake.
Nawe Yerusalema uliyeachwa tupu, kwa nini sasa unavaa nguo nzuri nyekundu? Kwa nini kujipamba kwa zahabu, na kujipakaa wanja kwenye macho? Unajipamba bure! Wapenzi wako wanakuzarau sana; wanatafuta kukuua tu.
Musifuate mwenendo wa siku hizi, lakini muache Mungu awabadilishe kwa kugeuza upya nia zenu, hata mukuwe na mawazo mapya. Kwa hiyo mutaweza kutambua mapenzi ya Mungu. Mutajua mambo gani yanayokuwa mema, yanayomupendeza Mungu na yanayokuwa makamilifu.