Kijana yule hakusita hata kidogo kutimiza sharti hilo, kwa vile alivyomupenda binti ya Yakobo, ingawa ni yeye ndiye aliyeheshimika kuliko wote katika nyumba yao.
Lakini Yebesi alimwomba Mungu wa Israeli akisema: “Ee Mungu, ninakusihi unibariki na kupanua mipaka yangu. Mukono wako ukuwe pamoja nami na unilinde kutokana na jambo lolote ovu, na mateso yasinipate.” Naye Mungu akamupa yale aliyoomba.
Ninyi ni wa bei kali mbele yangu, ninawaheshimu na kuwapenda. Kwa hiyo, ninatoa watu kusudi niwapate ninyi, ninayaachilia mataifa pahali pa maisha yenu.
Watu hao walikuwa wenye nia nzuri zaidi kuliko watu wa Tesalonika; nao walipokea Neno la Mungu kwa hamu kubwa. Kila siku walichunguza Maandiko Matakatifu wapate kujua kwamba maneno Paulo aliyosema yalikuwa ya haki.
Naye akamwita mutoto wake Ikabodi, maana alisema: “Utukufu wa Mungu umeondolewa kwa Waisraeli”, akiwa na maana kwamba Sanduku la Agano lilikuwa limetekwa, tena baba mukwe wake na mume wake, wote walikufa.