Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Mambo ya Siku 22:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Daudi akatoa amri kwamba wageni wote waliokuwa katika inchi ya Israeli wakusanyike, naye akawapangia kazi. Akaweka wamoja wachonge vizuri mawe ya kujenga nyumba ya Mungu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Mambo ya Siku 22:2
16 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kisha, mufalme Hiramu wa Tiro alituma wajumbe kwa Daudi. Alimupelekea vilevile miti ya mierezi, waseremala na wajengaji ambao walimujengea Daudi nyumba ya kifalme.


Wakati nyumba ilipokuwa inajengwa, hakukusikilika ndani ya nyumba mulio wa nyundo, wala wa chombo chochote cha chuma, maana ilijengwa kwa mawe yaliyokuwa yamechongwa na kutayarishwa kabisa kule walikoyachimba.


Halafu kisha kuzipima walizitoa kwa wafanyakazi waliosimamia nyumba ya Yawe, nao wakazilipa kwa waseremala na wenye kujenga waliotengeneza nyumba ya Yawe,


waseremala, wajengaji na watumishi wengine wenye kujenga, na kununua mbao na mawe yaliyochongwa kwa ajili ya kutengeneza nyumba.


Kisha mufalme Hiramu wa Tiro akatuma wajumbe kwa Daudi, akamupelekea vilevile miti ya mierezi, wajengaji na waseremala, kusudi wamujengee Daudi nyumba ya kifalme.


Mufalme Daudi akawaambia wale watu wote waliokusanyika: “Solomono mwana wangu, ambaye peke yake amechaguliwa na Mungu, angali bado mudogo, hana maarifa mengi na kazi hii ni kubwa. Nyumba atakayojenga si ya mwanadamu, lakini ni ya Mungu, Yawe.


Mufalme Solomono akawahesabu wageni wote waliokuwa katika inchi ya Israeli. Hesabu hii ni kama ile Daudi baba yake aliyofanya. Kulikuwa wageni yapata elfu mia moja makumi tano na tatu na mia sita.


Kati yao akawapa watu elfu makumi saba kazi ya kubeba mizigo, watu elfu moja wakakuwa wachongaji wa mawe kwenye milima, na watu elfu tatu mia sita wakakuwa wasimamizi kusudi wawasukume watu kufanya kazi.


Watu walitoa feza za kuwalipa waseremala na wajengaji, walitoa vilevile chakula, vinywaji na mafuta, kusudi vipelekwe katika miji ya Tiro na Sidona kubadilishwa na miti ya mierezi kutoka Lebanoni. Miti hiyo ililetwa kwa njia ya bahari mpaka Yopa. Haya yote yalifanyika kwa musaada wa mufalme Kiro wa Persia.


Kwa wakati ule mulikuwa mumetengwa mbali na Kristo. Hamukukuwa kati ya watu waliochaguliwa na Mungu, mulikuwa wageni kati yao. Ninyi hamukukuwa na pato lolote katika agano zile Mungu alizotoa katika ahadi yake kwa watu wake. Muliishi katika dunia pasipo tumaini wala kumujua Mungu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ