Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Zefania 3:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Kwa hiyo muningojee mimi Yawe, ngoja siku nitakaposimama kutoa mashitaki. Nimeamua kuyakusanya mataifa na falme, kuyamwangia kasirani yangu, na ukali wa hasira yangu. Dunia yote itateketezwa kwa moto wa kasirani yangu.

Gade chapit la Kopi




Zefania 3:8
39 Referans Kwoze  

Hata juu ya watumishi wanaume na wanawake, nitashusha Roho wangu wakati huo.


Feza yao wala zahabu yao havitaweza kuwaokoa katika siku hiyo ya kasirani ya Yawe. Kwa moto wa wivu wake dunia yote itateketezwa. Kwa ukamilifu na kwa namna ya kuogopesha atawafanya wakaaji wote katika dunia watoweke.


Lakini mimi ninamutumainia Yawe, ninamutazamia Mungu mwenye kuniokoa; Mungu wangu atanisikiliza.


Umutegemee Yawe! Ujitie moyo, ukuwe hodari! Umutegemee Yawe!


Siku Bwana atakaporudi, itatimia kama vile mwizi anavyokuja. Siku ile mbingu zitatoweka kwa shindo kubwa, na viumbe vyote vinavyoangaza katika mbingu vitayeyuka. Dunia na vitu vyote vinavyokuwa ndani yake vitateketezwa.


Hawa ndio pepo wanaoonyesha vitambulisho. Nao ndio wanaokwenda kwa wafalme wote wa dunia na kuwakusanya kwa kupigana vita Siku ile kubwa ya Mungu Mwenye Uwezo.


Mataifa yote yatakusanyika mbele yake, naye atayatenga kwa makundi mawili kama vile muchungaji anavyotenga kondoo na mbuzi.


Maono haya yanangoja wakati uliopangwa; ni maono ya ukweli juu ya mwisho. Kama yanaonekana kuchelewa, uyangojee; hakika yatafika, wala hayatachelewa.


Yawe wa majeshi, Yawe, ndilo jina lake.


Hata hivyo, Yawe anangoja kuwasamehe, atasimama na kuwaonea huruma. Yawe ni Mungu wa haki. Heri wote wale wanaomutumainia.


Unipige kama muhuri ndani ya moyo wako, kama muhuri katika mikono yako. Maana mapendo yana nguvu kama kifo, nao wivu ni mukali kama kaburi. Kuwaka kwake ni kama kuwaka kwa moto, unawaka kama ulimi wa moto.


Usiseme: “Nitalipiza ubaya niliotendewa.” Umutegemee Yawe naye atakusaidia.


Kama watumishi wanavyomutegemea bwana wao, kama mujakazi anavyomutegemea bibi mukubwa wake, ndivyo nasi tunavyokutegemea wewe, ee Yawe, Mungu wetu, mpaka hapo utakapotuonea huruma.


Mumepanga kuniangusha toka nafasi yangu ya heshima; furaha yenu ni kusema uongo. Kwa maneno, munabariki, lakini ndani ya moyo munalaani.


Kwa mukubwa wa waimbaji. Kwa mutindo wa Yedutuni. Zaburi ya Daudi.


Umutumainie Yawe na kushika njia yake, naye atakuinua uirizi inchi, na kuwaona waovu wakiongolewa.


Tulia mbele ya Yawe, umungojee kwa uvumilivu; usihangaike juu ya wale wanaofanikiwa, ndio watu wanaojaliwa katika mipango yao mibaya.


Wao wanasema: “Kwa ndimi zetu tutashinda; tuko na midomo, nani anayeweza kututawala?”


Kisha nikasikia sauti kubwa ikitoka katika hekalu ikiwaambia wale wamalaika saba: “Mwende kumwanga vile vikombe saba vya kasirani ya Mungu juu ya dunia!”


Ee Yawe, utakasirika hata milele? Hasira yako itawaka kama moto hata wakati gani?


Uyamwangie mataifa yasiyokujua hasira yako, ndizo, tawala zote zisizoheshimu jina lako.


Huu ndio uamuzi wa Yawe juu ya dunia yote; hii ndiyo azabu atakayotoa juu ya mataifa yote.


Umwange hasira yako juu ya mataifa yasiyokuabudu, na juu ya watu ambao hawakutambui. Maana, wamewaua wazao wa Yakobo; wamewaua na kuwaangamiza kabisa, na inchi yao wameiacha mabomoko.


na kuangusha falme na kukomesha nguvu zao. Nitayapindua magari yao ya vita na waaskari wapanda-farasi wake, nao wataanguka na kuuana wao kwa wao.


Yawe amekasirikia mataifa yote, amekasirikia majeshi yao yote. Ameyapangia mwisho wao, ameyatoa yaangamizwe.


Kwa hasira yangu niliwaponda watu, niliwalewesha kwa kasirani yangu; damu yao niliimwanga chini.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite