Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Zefania 3:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Nilisema: Hakika katika muji huu watanitii na kukubali kuonywa; hawataacha kukumbuka mara hizo zote nilizowaazibu. Lakini watu wake walizidisha tamaa zao za kufanya matendo yao kuwa upotovu.

Gade chapit la Kopi




Zefania 3:7
25 Referans Kwoze  

Ninyi mumezama katika uovu, kama ilivyokuwa kule Gibea. Mungu atayakumbuka makosa yao, na kuwaazibu kwa ajili ya zambi zao.


Labda watu wa Yuda watasikia juu ya hasara zote ambazo nimekusudia kuwatendea, kusudi kila mumoja wao auache mwenendo wake mubaya, nami nipate kuwasamehe makosa yao na zambi yao.


Hausikilizi onyo lolote, wala haukubali kutii. Haukumutegemea Yawe hata kidogo, wala kumukaribia Mungu wake.


Wao waliwaambia hivi: Kila mumoja wenu aachane na mwenendo wake mwovu na matendo yake mabaya, kusudi mupate kuishi katika inchi ambayo Yawe amewapa ninyi na babu zenu tangu zamani kuwa urizi wenu milele.


Mukifanya hivyo, mimi nitawaacha mukae siku zote pahali hapa, katika inchi niliyowapa babu wenu tangu zamani.


Bwana hakawii kutimiza ahadi zake kama vile watu wamoja wanavyozania. Yeye anavumilia kwa ajili yenu, maana hapendi hata mutu mumoja apotee, lakini anataka watu wote wageuke toka zambi zao.


Hapo Yeremia akamwambia Zedekia: Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Kama ukijitoa mwenyewe na kujitia katika mikono ya wakubwa wa mufalme wa Babeli, utayaokoa maisha yako na muji hautateketezwa kwa moto; nawe pamoja na jamaa yako mutaendelea kuishi.


Mimi nilisikiliza kwa uangalifu, lakini wao hawakusema ukweli wowote. Hakuna mutu anayetubu uovu wake, wala kujiuliza hivi: Nimefanya nini? Kila mumoja wao anashika njia yake, kama farasi anavyokimbia haraka kwa vita.


Maana alisema juu yao: Hakika, hawa ni watu wangu; watoto wangu ambao hawatanidanganya. Basi yeye akakuwa Mwokozi wao.


Ni kitu gani nilichokosa kulifanyia shamba langu? Nilipotazamia lizae zabibu nzuri, mbona basi, likazaa zabibu chungu?


Kwa hiyo, Yawe akawaleta majemadari wa jeshi la mufalme wa Asuria. Hao majemadari wakamukamata Manase kwa ndoana, wakamufunga kikomo cha shaba, wakamupeleka mpaka Babeli.


musipotoke kwa kujifanyia sanamu yoyote ya kuchonga, au ya umbo au mufano wowote, mufano wa wanaume au wanawake,


Mungu aliangalia dunia, akaona kwamba imeharibika kabisa, kwa maana kila mutu alifuata njia yake mbaya.


Shabaha ya agizo hilo ni kusudi kuwe upendo unaotokana na moyo safi na zamiri nzuri na imani ya kweli.


Anafungua masikio wasikie mafundisho, na kuwaamuru warudi na kuacha uovu.


Mungu anasema: “Nitakufundisha na kukuonyesha njia utakayofuata. Nitakushauria kwa uangalifu mukubwa.


Sikiliza shauri na kupokea mafundisho, upate hekima ya kukufaa kwa siku zinazokuja.


Basi usikilize maonyo, ee Yerusalema. Kama sivyo nitakutupilia mbali; nitakufanya ukuwe jangwa, kuwa pahali pasipokaliwa na mutu.


Ingawa hivyo babu zenu hawakunisikiliza wala kunitegea sikio, lakini walifanya vichwa vyao kuwa vigumu, wakakataa kusikia na kufuata maagizo yangu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite