Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Zefania 3:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

17 Yawe, Mungu wako, yuko pamoja nawe. Yeye ni shujaa anayekuletea ushindi. Yeye atakufurahia kwa furaha kubwa. Kwa upendo wake atakujalia uzima mupya. Atakufurahia kwa wimbo wa sauti kubwa,

Gade chapit la Kopi




Zefania 3:17
30 Referans Kwoze  

Maana Yawe anapendezwa na watu wake; yeye anawaheshimisha wanyenyekevu kwa kuwapa ushindi.


lakini anapendezwa na watu wanaomuheshimu, ndio wanaotegemea wema wake.


Nitafurahi kuwatendea mema; nitawasimika siku zote katika inchi hii na kuwatendea kwa uaminifu.


Ni kwa sababu hii anaweza kuwaokoa kabisa wao wanaokuja kwa Mungu kwa njia yake, kwa maana yeye anaishi siku zote kusudi akuwe mwombezi mbele ya Mungu.


Mungu ndiye mwenye kuniokoa, nitamutegemea yeye, wala sitaogopa; Yawe ananijalia nguvu; yeye mwenyewe ndiye anayeniokoa.


Yawe, Mungu wenu, atawafanya mufanikiwe katika kila mutakalofanya; mutakuwa na watoto wengi na ngombe wengi na mashamba yenu yatatoa mazao. Maana atapenda tena kuwafanya mufanikiwe kama vile alivyopenda kuwafanikisha wazee wenu,


Yawe amekuondolea hukumu iliyokuwa juu yako, amewafukuza waadui zako. Yawe, mufalme wa Israeli yuko pamoja nawe. Hautaogopa tena hasara.


“Nimewaambia ninyi maneno haya kusudi mufurahi sawa mimi, na furaha yenu ikuwe kubwa kabisa.


Nami nitaufurahia Yerusalema, nitawafurahia watu wangu. Sauti ya kilio haitasikilika tena, kilio cha taabu hakitakuwa tena.


Ikiwa Yawe amependezwa nasi, atatupeleka huko na kutupatia inchi inayotiririka maziwa na asali.


Mupige vigelegele na kuimba kwa furaha, enyi wakaaji wa Sayuni, maana Mutakatifu wa Israeli ni makubwa kati yenu.


Kwa hivi ilitupasa kushangilia na kufurahi, kwa maana mudogo wako huyu alikuwa amekufa na amefufuka, alikuwa amepotea na sasa ameonekana.’ ”


Lakini Yawe anayekuwa katika muji ule ni mwenye haki, yeye hatendi jambo lolote baya. Kila siku asubui anatangaza hukumu yake, kila kunapopambazuka anaitimiza. Lakini waovu hawana haya hata kidogo.


Kulikuwa kumebaki siku moja mbele ya kutimia kwa sikukuu ya Pasaka. Yesu alijua kwamba saa yake ya kutoka katika dunia na kurudi kwa Baba yake imetimia. Yeye alikuwa akiwapenda watu wake waliokuwa katika dunia, na akaendelea kuwapenda mpaka mwisho.


Utawala wake utastawi siku zote, amani ya ufalme wake haitakoma. Atakamata madaraka ya mufalme Daudi na kutawala juu ya ufalme wake; ataustawisha na kuuimarisha kwa kufuata sheria ya Mungu na kutenda kwa haki tangu sasa na hata milele. Yawe wa majeshi atafanya mambo hayo.


Kuna jambo lolote lisilowezekana kwa Yawe? Nitakurudilia wakati uliopangwa, kwa wakati kama huu katika mwaka, na Sara atakuwa na mutoto mwanaume.”


Maana, Yawe ameniambia hivi: Tokea juu kwenye makao yangu nitaangalia yanayotukia, nikitulia kama joto katika mwangaza wa jua, kama wingu la umande wakati wa mavuno.


Wakati Abramu alipokuwa na umri wa miaka makumi tisa na tisa, Yawe akamutokea, akamwambia: “Mimi ni Mungu Mwenye Uwezo. Uendelee mbele yangu na kuwa mukamilifu.


Mungu akaona kwamba kila kitu alichofanya ni kizuri kabisa. Ikakuwa magaribi na kisha ikakuwa asubui, ndiyo siku ya sita.


Ni nani huyu anayekuja kutoka Edomu, anayefika kutoka Bosira na nguo ya madoa mekundu? Ni nani huyo aliyevaa nguo ya utukufu, anatembea kwa nguvu zake kubwa? Ni mimi Yawe ninayetangaza ushindi wangu; nami ni mwenye nguvu ya kuokoa.


ambaye kwa mukono wake wenye nguvu alifanya maajabu kwa njia ya Musa, akapasua bahari na kuwaongoza watu wake, na kujipatia jina la milele?


Kwa siku ya saba Mungu alikuwa amemaliza kazi yake yote aliyofanya. Kwa siku ile ya saba Mungu akapumzika kisha kazi yake yote aliyofanya.


Inchi ya Asuria haitatuokoa, hatutategemea tena farasi wa vita. Hatutaziita tena Mungu wetu hizo sanamu tulizochonga. Kwako, ee Mungu, yatima anapata huruma.


Usiogope, ewe inchi, lakini ufurahi na kushangilia, maana Yawe ametenda mambo makubwa.


Kambi yenu inapaswa kuwa takatifu kwa sababu Yawe, Mungu wenu anatembea katika kambi yenu kusudi awaokoe na kuwatia waadui zenu katika mikono yenu. Kwa hiyo musimwache aone kitu chochote kisichofaa kati yenu, kama sivyo atawaacha ninyi.


Kisha Bwana aliamuka kama kutoka katika usingizi, kama shujaa aliyechangamushwa na divai.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite