Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Zefania 3:15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

15 Yawe amekuondolea hukumu iliyokuwa juu yako, amewafukuza waadui zako. Yawe, mufalme wa Israeli yuko pamoja nawe. Hautaogopa tena hasara.

Gade chapit la Kopi




Zefania 3:15
48 Referans Kwoze  

Bwana, Yawe, Mungu wako, anayewatetea watu wake, anasema hivi: Nimekuondolea kikombe cha kuyumbisha, hautakunywa tena kikombe cha kasirani yangu.


Nitakapowajaza Waisraeli Roho yangu, sitageuka tena wasipate kuniona. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.–


Lakini Yawe anayekuwa katika muji ule ni mwenye haki, yeye hatendi jambo lolote baya. Kila siku asubui anatangaza hukumu yake, kila kunapopambazuka anaitimiza. Lakini waovu hawana haya hata kidogo.


Nitawasimika katika inchi yao, wala hawataongolewa tena kutoka katika inchi niliyowapa. –Ni Yawe anayesema hivyo.


Natanaeli akamwambia tena: “Mwalimu, wewe ni Mwana wa Mungu, wewe ni Mufalme wa Waisraeli.”


Muji Yerusalema utakaliwa na watu maana ndani yake hakutakuwa laana tena; watu watakaa kule kwa usalama.


Siku hiyo nitaufanya Yerusalema kuwa kama jiwe zito kwa watu wote: yeyote atakayelinyanyua atajiumiza mwenyewe. Watu wa mataifa yote katika dunia wataushambulia muji ule.


Mateso makali hayatasikilika tena katika inchi yako; wala uharibifu na maangamizi ndani ya mipaka yako. Utaweza kuziita kuta zako: “Wokovu”, na milango yako: “Sifa”.


Maana Yawe ni mwamuzi wetu, yeye ni mutawala wetu; Yawe ni mufalme wetu, yeye ndiye anayetuokoa.


Umewasamehe watu wako kosa lao; umefuta zambi zao zote.


Kisha nikasikia sauti kubwa kutoka mbinguni, ikisema: “Sasa wokovu, uwezo na ufalme wa Mungu, na mamlaka ya Kristo wake vimefika. Ni vile, kwa yule aliyekuwa akiwashitaki wandugu zetu mbele ya Mungu wetu muchana na usiku ametupwa chini ya mbingu.


Ndiyo maana wanasimama mbele ya kiti cha kifalme cha Mungu, nao wanamutumikia muchana na usiku katika hekalu lake. Na yule anayeikaa juu ya kiti cha kifalme atawalinda katika hema yake.


Pilato akaamuru andiko liandikwe na kuwekwa juu ya musalaba. Nalo liliandikwa hivi: “Yesu wa Nazareti, Mufalme wa Wayuda.”


“Musiogope ninyi wakaaji wa Sayuni! Angalia, mufalme wenu anakuja, akipanda juu ya mwana-punda.”


Mushangilie sana enyi watu wa Sayuni! Mupige vigelegele, enyi watu wa Yerusalema! Angalia, mufalme wenu anawakujia, anakuja kwa shangwe na ushindi! Ni mupole, amepanda juu ya punda, juu ya mwana-punda, mutoto wa punda.


Yawe, Mungu wako, yuko pamoja nawe. Yeye ni shujaa anayekuletea ushindi. Yeye atakufurahia kwa furaha kubwa. Kwa upendo wake atakujalia uzima mupya. Atakufurahia kwa wimbo wa sauti kubwa,


Mateso uliyoyatenda kule Lebanoni yatakulemea wewe; uliwaua nyama, nyama nao watakuogopesha. Yote hayo yatakupata wewe, kwa mauaji na mateso uliyoitendea dunia, uliyoifanyia miji na wakaaji wake wote.


Halafu adui yangu ataona hayo naye atafunikwa na haya; maana aliniambia: Basi Yawe, Mungu wako, yuko wapi? Mimi mwenyewe nitamwona adui akianguka; atakanyagwakanyagwa chini kama matope katika njia.


Jumla ya urefu wa kuta zote ine utakuwa ni metre elfu kenda. Jina la muji kutokea sasa na kuendelea litakuwa: Yawe Yupo Hapa.


Nami nitaufurahia Yerusalema, nitawafurahia watu wangu. Sauti ya kilio haitasikilika tena, kilio cha taabu hakitakuwa tena.


Utaimarishwa katika haki, mbali na kaoneo, nawe hautaogopa kitu; mbali na hofu, maana haitakukaribia.


Bwana wetu Yawe atakiangamiza kifo milele! Atayafuta machozi katika nyuso za watu wote na kuondoa haya ya watu wake katika dunia yote. Yawe amesema hivyo.


Rakeli akapata mimba, akazaa mutoto mwanaume, akasema: “Mungu ameniondolea haya yangu.”


Na juu ya nguo yake na paja la muguu wake kulikuwa kumeandikwa jina hili: “Mufalme wa wafalme na Bwana wa wabwana.”


Wewe umenyanganya mataifa mengi, lakini wote wanaobaki watakunyanganya wewe, kwa mauaji na mateso uliyoitendea dunia, uliyoifanyia miji na wakaaji wake wote.


Waliokombolewa na Yawe watarudi, watakuja Sayuni wakipiga vigelegele. Watakuwa wenye furaha ya milele, watajaliwa furaha na shangwe; huzuni na kilio vitatoweka kabisa.


“Siwezi kufanya kitu kwa mafikiri yangu mwenyewe. Ninahukumu tu kama vile Mungu anavyoniambia na hukumu yangu ni ya haki, kwa sababu sitafuti kufanya mapenzi yangu, lakini mapenzi ya yule aliyenituma.


Enyi mbingu, nanyi watu wa Mungu pamoja na mitume na manabii wake, mufurahi kwa ajili ya mambo yaliyotokea muji ule, kwa maana Mungu amewapatia haki yenu kwa kuuhukumu!


Kanuni za Yawe ni sawa; zinafurahisha moyo. Amri za Yawe ni safi; zinamufungua mutu macho.


Mupige vigelegele na kuimba kwa furaha, enyi wakaaji wa Sayuni, maana Mutakatifu wa Israeli ni makubwa kati yenu.


Wewe ulisema kwamba mataifa hayo mawili, ni kusema inchi ya Yuda na ya Israeli, ni mali yako na kwamba utazirizi! Ulisema hivyo ingawa humo ni makao yangu mimi Yawe.


Umufurahie Muumba wako, ee Israeli; ninyi wakaaji wa Sayuni, mumushangilie mufalme wenu.


Mupige kelele za shangwe, enyi mabomoko ya Yerusalema! Yawe amewafariji watu wake, ameukomboa Yerusalema.


Sikiliza kilio cha watu wangu, kutoka kila upande katika inchi. Yawe hayuko tena katika Sayuni? Mufalme wa Sayuni hayuko tena? Lakini Yawe anasema: Mbona wamenikasirikisha na sanamu zao za kuchongwa, nayo miungu yao ya kigeni?


Sitaruhusu tena mataifa yawatukane, wala kuwazarau tena. Hamutasababisha taifa lenu kukosa. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite