Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Zefania 3:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Ole wake Yerusalema, muji wa uasi, muchafu, na wenye kujaa watesaji.

Gade chapit la Kopi




Zefania 3:1
17 Referans Kwoze  

Yawe wa majeshi anasema hivi: Mukate miti na kulundika udongo, kwa kuweza kupandia ndani ya Yerusalema. Muji huu unapaswa uazibiwe, maana hamuna lolote ndani yake isipokuwa ukorofi tu.


Tumekuasi na kukukana, ee Yawe, tumekataa kukufuata, ewe Mungu wetu. Tunasema maneno ya kutesa na uasi, katika mioyo yetu tunatunga na kutoa maneno ya uongo.


Kwa hiyo Mungu, Mutakatifu wa Israeli, anasema hivi: Ninyi mumeukataa ujumbe wangu; mukatumainia kutenda mabaya na kutengeneza udanganyifu.


Yawe wa majeshi anasema: Kisha nitawakaribia kwa kuwahukumu. Sitasita kutoa ushuhuda juu ya wachawi, wazinzi, watoa ushuhuda wa uongo, wanaopunja mushahara wa watumishi, wanaowatesa wajane na wayatima, wanaozuia mugeni asipate haki yake na wale wasioniogopa mimi.


Musiwatese wajane, wayatima, wageni au wamasikini; musipange kutendeana mabaya ndani ya mioyo yenu.


Kwako baba na mama wanazarauliwa. Mugeni anayekaa kwako ananyanganywa mali yake. Wayatima na wajane wanaonewa.


Wanatamani mashamba na kuyatwaa; wakitaka nyumba, wananyanganya. Wanawatesa wenye nyumba na jamaa zao, wanawanyanganya watu mali zao.


Lakini macho yako wewe na moyo wako, vinaelekea tu mapato yasiyokuwa ya haki. Unamwanga damu ya wasiokuwa na kosa, nawe unawatesa watu na kuwatendea kwa ukali.


Shamba la mizabibu la Yawe wa majeshi ni taifa la Waisraeli, na mizabibu mizuri aliyoipanda ni watu wa Yuda. Yeye alitazamia watu wafuate sheria yake, akaona mauaji; alitazamia haki, alisikia kilio!


Kibofu chake pamoja na uchafu wake ataviondoa na kuvitupa upande wa mashariki wa mazabahu ambako majivu yanawekwa.


Musikilize neno hili, enyi wanawake munaokuwa kama ngombe wa Basani munaokuwa kule juu ya mulima wa Samaria. Ninyi munaowaonea wamasikini, munaowagandamiza wakosefu, na kuwaambia waume zenu: Mutuletee divai tukunywe! Musikilize ujumbe huu:


Mutangaze katika nyumba nzuri kule Asidodi, na katika nyumba nzuri za inchi ya Misri: Mukusanyike kwenye milima inayoizunguka inchi ya Samaria, mujionee fujo kubwa na mateso yanayofanyika kule.


ndivyo vilivyokuletea hali hiyo. Wewe ulizini na mataifa, ukajichafua kwa kuabudu miungu yao.


Kila fasi katika inchi watu wanatendeana vibaya na kunyanganya kwa kinguvu. Wanagandamiza wamasikini na wakosefu, na kuwaonea wageni bila kujali.


Lakini watu hawa wana moyo mugumu na wa uasi; wamegeuka na kuniacha.


Wavu wenu haufai kama nguo, watu hawawezi kujifunikia munachofuma. Kazi zenu ni kazi za uovu, matendo yenu yote ni mateso makali.


Kama vile maji yanavyotiririka toka ndani ya kisima, ndivyo maovu yanavyotiririka katika Yerusalema. Mateso makali na maangamizi yanasikilika ndani yake. Ninaona magonjwa na vidonda mbele yangu kila siku.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite