Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Zefania 2:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Inchi ya pembeni ya bahari itakuwa makao ya mabaki ya ukoo wa Yuda. Watachunga nyama wao kule. Nyumba za muji wa Askeloni zitakuwa pahali pao pa kulala. Maana mimi Yawe, Mungu wao nitawakumbuka na kuwarudishia hali yao njema.

Gade chapit la Kopi




Zefania 2:7
42 Referans Kwoze  

Wakati huo nitawakusanya, na kuwafanya mujulikane na kusifiwa kati ya watu wote katika dunia, na kuwarudishia hali yenu njema, nanyi mutaona kwa macho yenu wenyewe. –Ni Yawe anayesema hivyo.


Kwa hiyo Bwana wetu Yawe anasema hivi: Sasa nitawahurumia Waisraeli wazao wa Yakobo, na kuwarudishia fanaka yao. Ninataka jina langu takatifu liheshimiwe siku zote.


Watu wakaamini. Na waliposikia kwamba Yawe amekuja kuwasaidia Waisraeli na kwamba ameyaona mateso yao, wote wakainamisha vichwa vyao na kumwabudu.


“Asifiwe Bwana, Mungu wa Waisraeli, maana amewasaidia watu wake na kuwakomboa.


Hao waliolemewa ndio watakaobaki wazima; hao waliopelekwa katika uhamisho watakuwa taifa lenye nguvu. Yawe atawatawala kwenye mulima Sayuni, tangu wakati ule na hata milele.


Lakini kweli nitawakusanya ninyi wote enyi watu wa Yakobo, nitawakusanya enyi Waisraeli muliobaki, niwalete pamoja kama kondoo katika zizi, kama kundi kubwa la kondoo katika shamba la malisho; nanyi mutakuwa kundi la watu wengi.


Wale wanaokaa Negebu wataurizi mulima wa wazao wa Esau, wale wanaokaa katika Shefela watarizi inchi ya Wafilistini. Waisraeli watarizi inchi za Efuraimu na Samaria na watu wa kabila la Benjamina watarizi inchi ya Gileadi.


Nitawastawisha tena Wayuda na watu wa Israeli; nitawaimarisha kama walivyokuwa hapo zamani.


mutaniona. Nitatengeneza upya maisha yenu na kuwakusanya kutoka mataifa yote na pahali pote nilipowasambaza. Nitawarudisha pahali nilipowaondoa wakati nilipowapeleka katika uhamisho. –Ni ujumbe wa Yawe.


Ni hivi vilevile kwa wakati huu wa sasa kunabaki wamoja ambao Mungu alichagua kwa neema yake.


Filipo akajikuta amekwisha kuwa katika muji Azoto. Kisha akapita katika miji yote akihubiri Habari Njema, mpaka alipofika katika muji Kaisaria.


Malaika wa Bwana akamwambia Filipo: “Ujitayarishe na uende upande wa kusini kupitia njia inayotelemuka toka Yerusalema kwenda katika muji Gaza, nayo ni njia watu wasiyozoea kupitia.”


Watu wote wakashikwa na woga, nao wakamutukuza Mungu, wakisema: “Nabii mukubwa ametokea tena kwetu! Mungu amekuja kuwasaidia watu wake.”


Enyi watu wa Sayuni, mulie na kugaagaa kama mwanamuke anayezaa! Maana sasa mutaondoka katika muji huu muende kukaa katika mbuga, mutakwenda mpaka Babeli. Lakini kule, mutaokolewa. Kule Yawe atawakomboa toka katika makucha ya waadui zenu.


Watu watanunua mashamba kwa feza, watazitia sahihi barua zake za ununuzi, watazipiga muhuri, na kuweka washuhuda katika inchi ya Benjamina, kandokando ya Yerusalema, katika miji ya Yuda, katika miji ya inchi ya milima, katika miji ya Shefela, na katika miji ya jangwa la Negebu. Maana nitawastawisha tena. –Ni ujumbe wa Yawe.


Maana Yawe anasema hivi: Mushangilie kwa furaha kwa ajili ya Yakobo, mupige vigelegele kwa ajili ya taifa kubwa, mutangaze, musifu na kusema: Yawe ameokoa watu wake, ameleta ukombozi kwa wale waliobaki kati ya Waisraeli!


Maana, siku zinakuja ambapo nitatengeneza upya maisha ya watu wangu wa Israeli na Yuda. –Ni Yawe anayesema.– Nitawarudisha katika inchi niliyowapa babu zao, nao watairizi.


Kisha, nitawakusanya kondoo wangu waliobaki kutoka inchi zote nilipowafukuza, na kuwarudisha katika malisho yao. Nao watazaa na kuongezeka.


Siku hizo, watu wa Yuda wataungana na watu wa Israeli, na wote kwa pamoja watatoka katika inchi ya kaskazini na kurudi katika inchi niliyowapa babu zenu ikuwe urizi wao.


Siku hiyo, Bwana ataunyoosha mukono wake tena kuwarudisha watu wake waliobaki kule Asuria, Misri, Patirosi, Etiopia, Elamu, Sinari, Hamati na sehemu za visanga vya bahari.


Kwa mukubwa wa waimbaji: Zaburi ya Wakora.


Kisha Yosefu akawaambia wandugu zake: “Mimi sasa ninakaribia kufa. Lakini Mungu hakika atawafikia kwa kuwasaidia. Atawatoa katika inchi hii na kuwapeleka katika inchi aliyowaapia Abrahamu, Isaka na Yakobo.”


Sema na mutawala wa Yuda, Zerubabeli mwana wa Saltieli, Kuhani Mukubwa Yoshua mwana wa Yosadaki na watu waliorudi kutoka katika uhamisho uwaambie hivi:


Halafu Zerubabeli mwana wa Saltieli, na Kuhani Mukubwa Yoshua mwana wa Yosadaki, pamoja na watu wote waliokuwa wamerudi kutoka katika uhamisho wakafanya kama vile Yawe, Mungu wao alivyowaambia na kama vile walivyoambiwa na Hagai, yule nabii aliyetumwa na Yawe, Mungu wao. Watu wakamuheshimia Yawe.


Kwa hiyo, kama vile ninavyoishi, –ni ujumbe wa Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli– inchi ya Moabu itakuwa kama Sodoma na ya Amoni itakuwa kama Gomora. Inchi zake zitakuwa shamba la miiba na mashimo ya chumvi, zitakuwa ukiwa milele. Watu wangu watakaobaki wataziteka, watu wa taifa langu waliobaki watazirizi.


Yawe atawahurumia tena watu wa Yakobo, atawachagua tena Waisraeli. Atawarudisha katika inchi yao wenyewe, na wageni watakuja na kukaa pamoja na watu wa Yakobo.


Kisha, Naomi akapata habari kwamba Yawe alikuwa amewabariki watu wake kwa kuwapa chakula. Basi, akaondoka kutoka Moabu kurudi kwao, pamoja na wakwe zake.


nguruwe wa mwitu wanauharibu, na wanyama wa pori wanautafuna!


Tena, kutakuwa barabara kubwa toka Asuria kwa ajili ya watu wake waliobaki humo kama ilivyokuwa kwa Waisraeli wakati walipotoka katika inchi ya Misri.


Maana nyumba ya kifalme itaachwa ukiwa, muji huo wa watu wengi utahamwa. Mulima na munara wa ulinzi utakuwa mapango milele, punda wa mwitu watapitapita huko kwa furaha, kondoo watapata malisho yao humo.


Yawe anasema hivi: Mutakapopitisha miaka makumi saba huko Babeli, nitawashugulikia na kuitimiza ahadi yangu ya kuwarudisha kwa nafasi hii.


Yawe wa majeshi anasema hivi: Pahali hapa ambapo ni jangwa bila watu wala nyama, na katika miji yake yote, patakuwa shamba ambalo wachungaji watakulisha ndani yake makundi yao ya kondoo.


Watu wa Gaza wamenyoa kichwa kwa kuomboleza; muji wa Askeloni umeangamia. Enyi watu muliobaki katika bonde mutajikatakata kwa huzuni mpaka wakati gani?


Nawe Yuda vilevile, nimekupangia wakati utakapovuna azabu.


Waisraeli watakaobaki hawatatenda mabaya wala hawatasema uongo, wala kwao hakutapatikana mudanganyifu yeyote. Watapata chakula na kulala wala hakuna mutu atakayewaogopesha.


Wote pamoja watashambulia Wafilistini wanaokuwa upande wa magaribi, pamoja watawanyanganya watu wanaokaa upande wa mashariki. Watawashinda Waedomu na Wamoabu, nao Waamoni watawatii.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite