Watatupa feza yao ndani ya barabara na zahabu yao itakuwa kama kitu kichafu. Feza na zahabu zao hazitaweza kuwaokoa katika siku hiyo ya kasirani ya Yawe; wala hawataweza kushiba au kujaza tumbo zao feza na zahabu waliyojilundikia; maana mali hiyo ndiyo iliyosababisha zambi yao.
Lakini niko na neno hili juu yako: kati yako kuna watu wamoja wanaoshika mafundisho ya Balama. Huyu ndiye aliyemufundisha Balaka kwamba awapime Waisraeli, kusudi wakule vyakula vya kutambikia sanamu za miungu na kufanya uasherati.
Wakati ule, nitaondoa majina ya sanamu za miungu katika inchi, wala hayatakumbukwa tena. –Ni ujumbe wa Yawe wa majeshi.– Na wanaojidai kuwa manabii nitawaondoa kabisa pamoja na tamaa zao za kuabudu sanamu.
Mpaka wakati gani inchi itaomboleza kwa kukauka, na nyasi za mashamba yote kunyauka? Nyama na ndege wanakufa kwa uovu wa wakaaji wake. Wao wanasema: Mungu hataona mwisho wetu.
Hivi ndivyo uovu wa wazao wa Yakobo utakavyoondolewa, hivi ndivyo zambi yake itakavyofutwa kabisa: ataziharibu mazabahu za miungu; mawe yake yatasagwasagwa kama chokaa. Sanamu za Ashera wala mazabahu za kufukizia ubani hazitabaki.
Lakini kwa sababu waliongoza ibada za miungu kwa ajili ya watu wa Israeli, wakasukuma watu kutenda zambi, basi, nimeunyoosha mukono wangu kuwaazibu. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.– Nao watabeba azabu yao.
Mwana wa Mutu atawatuma wamalaika wake, nao watakusanya toka katika Ufalme wake watu wote wanaowaangusha wengine katika zambi pamoja na wote wanaofanya maovu.
Mimi nikauliza: Bwana, mpaka wakati gani? Naye akanijibu: Mpaka wakati miji itakapobaki tupu bila wakaaji, nyumba bila watu, na inchi itakapoharibiwa kabisa.
Yawe anasema: Nitaifanya Yerusalema kuwa mabomoko matupu, nitaifanya kuwa pango la mbweha; na miji ya Yuda nitaifanya kuwa jangwa, pahali pasipokaliwa na mutu yeyote.
Kwa maana, taifa kutoka kaskazini limefika kuushambulia; litaifanya inchi yake kuwa uharibifu. Hakuna atakeyeishi humo; watu na nyama watakimbia mbali.
Hivyo akasema: “Nitamuharibu kabisa katika dunia mwanadamu niliyemwumba, pamoja na nyama wa pori, viumbe vinavyotambaa na ndege wa anga. Ninasikitika kwamba niliwaumba katika dunia.”
Kwa hiyo, Bwana wetu Yawe anasema hivi: Nitaimwanga hasira yangu juu ya pahali hapa, juu ya wanadamu na nyama, miti katika mashamba na juu ya mazao ya inchi. Nayo nafasi hii itawaka moto wala hautaweza kuzimishwa.