Zefania 1:15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
15 Siku hiyo itakuwa siku ya kasirani, ni siku ya taabu na uchungu, siku ya giza na huzuni; siku ya uharibifu na maangamizi, siku ya mawingu na giza kubwa.
Hiyo ni siku ya giza na huzuni; siku ya mawingu na giza nene. Jeshi kubwa linakaribia kama giza linalofunikia milima. Namna hiyo haijapata kuwa hata kidogo wala haitaonekana tena katika vizazi vyote vinavyokuja.
Maana leo Yawe wa majeshi ametuletea fujo, kushindwa na wasiwasi katika Bonde la Maono. Kuta za muji zimebomolewa. Kilio cha wakaaji wake kinasikilika mpaka kwenye milima.
Lakini kwa nguvu ya neno lile lile, mbingu na dunia za sasa zimewekwa akiba kwa kuteketezwa kwa moto. Zinalindwa kwa ajili ya Siku ile ambayo watu wabaya watahukumiwa na kuangamizwa.
Feza yao wala zahabu yao havitaweza kuwaokoa katika siku hiyo ya kasirani ya Yawe. Kwa moto wa wivu wake dunia yote itateketezwa. Kwa ukamilifu na kwa namna ya kuogopesha atawafanya wakaaji wote katika dunia watoweke.
Yawe anaamuru kundi lake kwa sauti; waaskari wake ni wengi sana, wanaomutii hawahesabiki. Siku ya Yawe kweli ni kubwa na ya kutisha sana! Nani atakayeweza kuivumilia?
“Mara moja kisha mateso ya siku zile, jua litatiwa giza, mwezi hautaangaza, nyota zitaanguka toka mbinguni na vyote vyenye nguvu katika mbingu vitatikiswa.
Watu hao watawazunguka katika miji yenu yote, mpaka kuta zenu za makimbilio ambazo mulitegemea zimeporomoshwa chini kila pahali katika inchi yenu ambayo Yawe, Mungu wenu, amewapa.