Yawe anaamuru kundi lake kwa sauti; waaskari wake ni wengi sana, wanaomutii hawahesabiki. Siku ya Yawe kweli ni kubwa na ya kutisha sana! Nani atakayeweza kuivumilia?
Kwa sababu amri itakapotoka na sauti ya malaika mukubwa itakaposikilika, na baragumu ya Mungu itakapolia, Bwana mwenyewe atashuka toka mbinguni. Halafu wale waliokufa wakimwamini Kristo watafufuliwa kwanza.
Na kwa sababu ya tamaa yao mbaya ya mali, walimu hawa wa uongo watajipatia faida juu yenu kwa njia ya maneno ya uongo. Lakini tangia zamani hukumu yao imekwisha kutangazwa, nao hawatakawia kuangamizwa.
Naye Yawe akaniuliza: Amosi, unaona nini? Nami nikamujibu: Ninaona kikapu cha matunda yenye kuivya. Kisha Yawe akaniambia: Mwisho umewafikia watu wangu wa Israeli. Sitavumilia tena maovu yao.
Mupige baragumu kule Sayuni; mupige kelele la kujulisha hatari kule juu ya mulima mutakatifu! Mutetemeke enyi wakaaji wa Yuda, maana siku ya Yawe inakuja, siku hiyo iko karibu!
Uwaambie kwamba Bwana wetu Yawe anasema kwamba nitakomesha mezali hiyo nao hawataitumia tena katika inchi ya Waisraeli. Uwaambie kwamba wakati umefika ambapo maono yote yatatimia.
Katika wakati ule sauti yake ilitetemesha dunia, lakini sasa ametuahidi hivi: “Nitatetemesha dunia mara moja tena, wala si dunia tu, lakini mbingu vilevile.”
Lakini mbona ninawaona wametishwa? Wamerudi nyuma. Mashujaa wao wamepigwa, wamekimbia mbio, bila hata kuangalia nyuma. Kuna kitisho kila upande. –Ni ujumbe wa Yawe.–