Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Zefania 1:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Hili ni neno la Yawe lililomufikia Zefania mwana wa Kusi, mujukuu wa Gedalia mwana wa Amaria, wa uzao wa mufalme Hezekia, wakati wa utawala wa mufalme Yosia mwana wa Amoni, mufalme wa Yuda:

Gade chapit la Kopi




Zefania 1:1
12 Referans Kwoze  

Neno la Yawe lilimufikia Yeremia katika mwaka wa kumi na tatu wa utawala wa Yosia mwana wa Amoni, mufalme wa Yuda.


Vilevile tunaamini ujumbe uliotangazwa na manabii. Ninyi munafanya vema mukishikamana nao. Ujumbe huo ni kama taa inayoangaza pahali pa giza, mpaka wakati wa mapambazuko na wakati nyota ya asubui itakapoangazia mioyo yenu.


Hili ni neno ya Yawe lililomufikia Hosea mwana wa Beri katika siku za utawala wa Uzia, Yotamu, Ahazi na Hezekia, wafalme wa Yuda, na Yeroboamu mwana wa Yoasi, mufalme wa Israeli.


neno la Yawe lilimufikia kuhani Ezekieli mwana wa Buzi, alipokuwa Babeli karibu na muto Kebari. Yawe alinijaza uwezo wake.


Kwa muda wa miaka makumi mbili na tatu sasa, ni kusema tangu mwaka wa kumi na tatu wa utawala wa mufalme Yosia, mufalme wa Yuda, mwana wa Amoni, mpaka hivi leo, nimekuwa nikipata neno la Mungu na kulitoa kwenu kila wakati, lakini ninyi hamukusikiliza.


Maandiko yote Matakatifu yameandikwa kwa maongozi ya Mungu na yanafaa kwa kufundisha, kuonya, kuhakikisha na kuadibisha katika haki,


Manase akakufa na kuzikwa katika bustani ya nyumba yake mwenyewe, katika Bustani ya Uza. Naye mwana wake Amoni akatawala kwa pahali pake.


Manase alikufa na kuzikwa katika nyumba yake ya kifalme, naye Amoni, mwana wake, akatawala pahali pake.


Maana, Yawe anasema hivi juu ya Salumu mwana wa Yosia, mufalme wa Yuda aliyetawala kwa pahali pa baba yake Yosia, na ambaye aliondoka pahali hapa: Salumu hatarudi tena pahali hapa,


Amoni akazikwa katika kaburi katika bustani ya Uza. Yosia mwana wake akatawala kwa pahali pake.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite