Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




ZAKARIA 9:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Mushangilie sana enyi watu wa Sayuni! Mupige vigelegele, enyi watu wa Yerusalema! Angalia, mufalme wenu anawakujia, anakuja kwa shangwe na ushindi! Ni mupole, amepanda juu ya punda, juu ya mwana-punda, mutoto wa punda.

Gade chapit la Kopi




ZAKARIA 9:9
43 Referans Kwoze  

Yawe anasema hivi: Mukimbie kutoka katika inchi ya kaskazini ambako mimi nilikuwa nimewatawanya kila upande.


Wakamuletea Yesu yule mwana-punda na kutandika nguo zao juu yake. Kisha Yesu akaikaa juu yake.


Mimi peke yangu ndiye Yawe, hakuna mukombozi mwingine isipokuwa mimi.


Mukubali kuongozwa nami kama vile ngombe dume anayefungiwa nira, nanyi mufuate mafundisho yangu maana mimi ni mupole na munyenyekevu. Kwa hiyo mutapumzika.


Kwenda juu ya mulima murefu, ewe Sayuni, utangaze habari njema. Lalamika kwa nguvu, ewe Yerusalema, utangaze habari njema. Lalamika bila kuogopa. Uambie miji ya Yuda: Muangalie: Mungu wenu!


Yawe ametangaza katika dunia yote, muwaambie watu wa Sayuni hivi: Mukombozi wenu anakuja, yeye anakuja na mapato yake, anafika na mushahara wake.


Maana mimi ni Yawe, Mungu wenu, Mungu Mutakatifu wa Israeli, Mwokozi wenu. Ninaitoa inchi ya Misri kwa ajili ya ukombozi wenu, ninaitoa Kushi na Seba kusudi muachwe huru.


Mupige vigelegele na kuimba kwa furaha, enyi wakaaji wa Sayuni, maana Mutakatifu wa Israeli ni makubwa kati yenu.


“Nimemusimika mufalme niliyemuchagua; anatawala Sayuni, mulima wangu mutakatifu!”


Natanaeli akamwambia tena: “Mwalimu, wewe ni Mwana wa Mungu, wewe ni Mufalme wa Waisraeli.”


Yeye atazaa mutoto mwanaume, nawe utamwita jina lake Yesu, kwa maana ndiye atakayewaokoa watu wake toka katika zambi zao.”


Nao hawatakuwa tena watumwa wa wageni, lakini watanitumikia mimi Yawe, Mungu wao pamoja na mufalme wa ukoo wa Daudi ambaye nitakayewasimikia.


Mutangaze na kusema habari zenu. Mufanye shauri pamoja! Ni nani aliyetangaza zamani matukio ya sasa? Ni nani aliyesema mambo haya zamani? Haikukuwa mimi Yawe? Hakuna Mungu mwingine isipokuwa mimi! Mimi ni Mungu wa haki na mwokozi; hakuna mwingine isipokuwa mimi.


Kwa mukubwa wa waimbaji. Kwa mutindo wa wimbo: “Mayungiyungi.” Mashairi ya Wakora. Wimbo wa mapenzi.


Lakini wakapiga kelele wakisema: “Umwue! Umwue! Umutundike juu ya musalaba!” Pilato akawauliza: “Munataka nimutundike mufalme wenu juu ya musalaba?” Wakubwa wa makuhani wakajibu: “Sisi hatuna mufalme mwingine isipokuwa Mufalme wa Roma.”


Nao wakauliza: “Yuko wapi yule mutoto aliyezaliwa kuwa mufalme wa Wayuda? Tumeona nyota yake inayomutambulisha, nasi tumekuja kumwabudu.”


Kisha akawaelezea maneno yaliyoandikwa juu yake katika Maandiko Matakatifu yote, akianza toka vitabu vya Musa na kuendelea katika vitabu vya manabii wote.


Yairi alikuwa na watoto wa kiume makumi tatu ambao walipanda juu ya punda makumi tatu na walikuwa na miji makumi tatu katika inchi ya Gileadi, ambayo mpaka leo inaitwa Miji ya Yairi.


Umufurahie Muumba wako, ee Israeli; ninyi wakaaji wa Sayuni, mumushangilie mufalme wenu.


Ujumbe wa Mungu juu ya nyama wa pande za jangwa ya kusini: Wajumbe wanapita katika inchi ya taabu na shida, yenye simba, nyoka wa sumu na nyoka wakubwa wanaoruka. Wamewabebesha punda na ngamia wao mali zao, kuwapelekea watu wasioweza kuwafalia kitu.


Maana Yawe ni mwamuzi wetu, yeye ni mutawala wetu; Yawe ni mufalme wetu, yeye ndiye anayetuokoa.


Hivi ndivyo anavyosema Mungu anayekuwa juu kabisa, anayeishi milele na ambaye jina lake ni Mutakatifu: Mimi ninakaa kule juu, Pahali Patakatifu, ninakaa vilevile na wenye majuto na wanyenyekevu. Mimi nitawatia moyo wanaokuwa wanyenyekevu na kuwapa nguvu wenye majuto.


Lakini nitawahurumia watu wa Yuda na kuwaokoa. Mimi Yawe, Mungu wao, nitawaokoa, lakini si kwa nguvu za waaskari, au pinde, au panga, au farasi au waaskari wapanda-farasi.


Hivyo Mungu atawaachilia watu wake kwa waadui, mpaka yule mwanamuke mwenye kuwa na mimba atakapozaa. Kisha wandugu zake waliobakia, watarudi na kuungana na Waisraeli wenzao.


Basi, kuhani Zadoki, nabii Natani na Benaya mwana wa Yehoyada, na Wakereti na Wapeleti, wote walishuka, wakamupandisha Solomono kwenye nyumbu wa mufalme Daudi, na kumupeleka mpaka Gihoni.


Ni furaha kabisa! Mujumbe anatokea kwenye mulima. Anatangaza habari njema za amani, heri, na ukombozi. Anauambia Sayuni: Mungu wako anatawala!


Uharibifu! Uharibifu! Hakuna chochote katika muji huu nitakachoacha. Lakini mbele ya hayo kutafika kwanza yule ambaye nimemupa mamlaka ya kuuazibu, ambaye mimi nitamupa muji ule.


Nawe kilima cha Yerusalema, wewe munara wa Sayuni, ambamo Mungu anafanya ulinzi juu ya watu wake, kama muchungaji juu ya kondoo wake, wewe utakuwa tena muji wenye mamlaka sawa zamani. Yerusalema utakuwa tena muji mukubwa wa mufalme.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite