Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




ZAKARIA 9:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Mimi mwenyewe nitailinda inchi yangu, nitazuia majeshi yasipitepite ndani. Hakuna mutu atakayewatesa tena watu wangu, maana, kwa macho yangu mwenyewe, nimeona jinsi walivyoteseka.

Gade chapit la Kopi




ZAKARIA 9:8
39 Referans Kwoze  

Utaimarishwa katika haki, mbali na kaoneo, nawe hautaogopa kitu; mbali na hofu, maana haitakukaribia.


Mateso makali hayatasikilika tena katika inchi yako; wala uharibifu na maangamizi ndani ya mipaka yako. Utaweza kuziita kuta zako: “Wokovu”, na milango yako: “Sifa”.


Amuka! Amuka! Ujipatie zile nguvu zako, ewe Sayuni! Uvae nguo yako nzuri, ewe Yerusalema, muji mutakatifu. Maana hawataingia tena kwako watu wasiotahiriwa na wachafu.


Watakuja na kuimba kwa sauti juu ya mulima Sayuni, watapata utukufu juu ya wema wangu mimi Yawe, kwa ajili ya ngano, divai na mafuta ninavyowapa, kwa ajili ya kondoo na ngombe vilevile; maisha yao yatakuwa kama bustani iliyotiliwa maji, wala hawataregea tena.


Nitawasimika katika inchi yao, wala hawataongolewa tena kutoka katika inchi niliyowapa. –Ni Yawe anayesema hivyo.


Nitakapowajaza Waisraeli Roho yangu, sitageuka tena wasipate kuniona. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.–


Mara hii hamutatoka kwa haraka, wala hamutaondoka mbiombio! Maana Yawe atawatangulia, Mungu wa Israeli atawalinda nyuma yenu.


Kama vile ndege anavyonyoosha mabawa juu ya vitoto vyake, ni vile Yawe atakavyolinda Yerusalema. Ataulinda na kuukomboa, ataukinga na kuuokoa.


Mufalme awatetee wamasikini wa taifa, awasaidie wakosefu, na kuwaangamiza watesaji.


Masikini alimulilia Yawe, naye akamusikia, na kumwokoa katika taabu zake zote.


Labda Yawe ataangalia mateso yangu, naye atanilipa wema kwa laana hii ninayopata leo.”


Hakika, kilio cha Waisraeli kimenifikia; nimeona jinsi Wamisri wanavyowatesa.


Walitawanyika katika dunia yote, na kuzunguka kambi ya watu wa Mungu na muji wake alioupenda. Lakini moto ukashuka toka mbinguni, ukawateketeza.


Hakika nimeona namna watu wangu Waisraeli wanavyoteswa katika inchi ya Misri. Nimesikia kilio chao nami nimeshuka kwa kuwaokoa. Sasa kuja, nitakutuma kule Misri.’


Muji Yerusalema utakaliwa na watu maana ndani yake hakutakuwa laana tena; watu watakaa kule kwa usalama.


Siku hiyo, mimi Yawe nitawalinda wakaaji wa Yerusalema. Wanaokuwa wazaifu zaidi kati yao watakuwa na nguvu kama mufalme Daudi. Wazao wa Daudi watashika usukani kwa kuwaongoza watu wa Yuda kama Mungu, au kama malaika wa Yawe.


Hili ndilo neno ambalo Yawe alimwambia Yeremia wakati Nebukadneza mufalme wa Babeli alipofika kuishambulia inchi ya Misri:


Juu ya Misri na jeshi la Neko mufalme wa Misri, lililokuwa huko Karkemisi karibu na muto Furati ambalo Nebukadneza mufalme wa Babeli alilishambulia katika mwaka wa ine wa utawala wa Yoyakimu mwana wa Yosia, mufalme wa Yuda:


Siku ile watu wataimba wimbo huu katika inchi ya Yuda: Sisi tuna muji imara: Mungu anatulinda kwa kuta na upango.


Halafu, kila pahali juu ya mulima Sayuni na juu ya mikutano ya watu atafanya kuwe wingu wakati wa muchana, na moshi na moto unaowaka vizuri wakati wa usiku. Zaidi ya hayo utukufu wa Mungu utaufunika na kuulinda muji wote.


Nebukadneza mufalme wa Babeli akaishambulia inchi ya Yuda. Yoyakimu akamutumikia kwa miaka mitatu halafu akaacha kumutii, akamwasi.


Wakati wa kutawala kwake, Neko mufalme wa Misri alikwenda mpaka kwenye muto Furati kwa kukutana na mufalme wa Asuria. Naye mufalme Yosia akaondoka kwa kupigana naye; lakini Neko mufalme wa Misri alipomwona akamwua kule Megido.


Kisha Yawe akamwambia: “Nimeona mateso ya watu wangu wanaokuwa katika inchi ya Misri na nimesikia kilio chao kinachosababishwa na watesaji wao. Ninajua mateso yao,


Nitawakomesha kula nyama yenye damu, na chakula ambacho ni chukizo. Watakaobaki watakuwa mali yangu, kama ukoo mumoja katika Yuda. Watu wa Ekroni watakuwa kama Wayebusi.


Kweli, kwa ajili ya heshima yangu mimi na kwa ajili ya mutumishi wangu Daudi, nitaulinda na kuukoa muji huu.”


Usiogope juu ya tisho la rafla, wala shambulio kutoka kwa waovu,


Siku hiyo, ninasema mimi Yawe, nitamutia hofu kila farasi, na askari mupanda-farasi wake nitamufanya kuwa mwenda-wazimu. Farasi wa mataifa mengine nitawapofusha. Lakini kabila la Yuda nitalilinda.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite