Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




ZAKARIA 9:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Nitawakomesha kula nyama yenye damu, na chakula ambacho ni chukizo. Watakaobaki watakuwa mali yangu, kama ukoo mumoja katika Yuda. Watu wa Ekroni watakuwa kama Wayebusi.

Gade chapit la Kopi




ZAKARIA 9:7
21 Referans Kwoze  

Kwa hiyo hakuna tena umbalimbali kati ya Wayuda na watu wa mataifa mengine, kati ya watumwa na watu huru, mwanaume na mwanamuke; kwa maana ninyi wote ni mumoja katika kuungana kwenu na Yesu Kristo.


Yawe wa majeshi anasema hivi: Wakati ule, watu kumi kutoka mataifa ya kila luga watamukamatilia Muyuda mumoja na kushika nguo yake na kumwambia: Tunataka kwenda pamoja nanyi, kwa sababu tumesikia kwamba Mungu yuko pamoja nanyi.


Yawe, anasema hivi: Kama vile muchungaji anavyonyanganya toka katika kinywa cha simba miguu miwili tu au kipande cha sikio la kondoo, ndivyo watu wachache tu wa Israeli wanaoishi Samaria, ambao sasa wanalalia vitanda vizuri na matandiko ya hariri watakavyobaki.


Lakini katika siku za mwisho, nitaurudishia muji wa Elamu hali yake. –Ni ujumbe wa Yawe!


Lakini kisha nitawarudisha tena Waamoni katika hali yao. –Ni ujumbe wa Yawe.


Lakini katika siku zinazokuja nitawarudisha tena Moabu katika hali yao. –Ni ujumbe wa Yawe. Hii ndiyo hukumu juu ya Moabu.


ambaye hasikii hata sauti ya mulozi, au ya muganga anayekuwa fundi wa uchawi.


Sitaogopa maelfu ya watu wanaonizunguka kila upande.


Halafu Mungu akatuma malaika aende kuharibu Yerusalema. Lakini mbele hajafanya vile, Yawe akageuza nia yake na kumwambia malaika yule aliyetimiza maangamizi: “Basi, inatosha!” Malaika alikuwa amesimama karibu na uwanja wa kupepetea ngano wa Ornani wa kabila ya Yebusi.


Muji wa Asidodi utakaliwa na wana haramu. Yawe anasema hivi: Nitakikomesha kiburi cha Wafilistini.


Mimi mwenyewe nitailinda inchi yangu, nitazuia majeshi yasipitepite ndani. Hakuna mutu atakayewatesa tena watu wangu, maana, kwa macho yangu mwenyewe, nimeona jinsi walivyoteseka.


Kanana vilevile ndiye babu ya Wayebusi, Waamori, Wagirgasi,


Wanaikaa katika makaburi na kupitisha usiku ndani ya mashimo. Wanakula nyama ya nguruwe na kuweka muchuzi wa nyama wachafu ndani ya sahani zao.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite