Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




ZAKARIA 9:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Lakini Bwana atatwaa mali yake yote, atautumbukiza utajiri wake katika bahari, na kuuteketeza muji ule kwa moto.

Gade chapit la Kopi




ZAKARIA 9:4
14 Referans Kwoze  

Kwa wingi wa mabaya yako na udanganyifu katika biashara yako ulipachafua pahali pako pa kuabudia; kwa hiyo niliwasha moto kwako, nao ukakuteketeza, nami nikakufanya kuwa majivu juu ya inchi, mbele ya wote waliokuangalia.


Watakuimbia wimbo huu wa kuomboleza: Namna gani wewe muji wenye utukufu, umetoweka kutoka katika bahari! Ulikuwa na nguvu juu ya bahari, wewe pamoja na wakaaji wako, wewe uliyeletea woga juu ya wote!


Basi, nitashusha moto juu ya kuta za muji wa Tiro, na kuziteketeza kabisa nyumba zake nzuri.


Ustawi wa biashara yako ulikujaza ukali, ukatenda zambi. Kwa hiyo nilikufukuza kama muchafu, mbali na mulima wangu mutakatifu. Na yule kerubi aliyekulinda akakufukuzia mbali na mawe yanayometameta.


Watakutumbukiza chini ndani ya shimo, nawe utakufa kifo cha rafla katika kilindi cha bahari.


Wewe mwanadamu! Umwambie mufalme wa Tiro kwamba Bwana wenu Yawe anasema hivi: Wewe una kiburi cha moyo, na umesema kwamba wewe ni mungu, kwamba umeikalia kiti cha kifalme cha miungu, umekaa mbali huko katika bahari. Lakini, wewe ni mutu tu wala si mungu, ingawa unajiona kuwa na hekima kama mungu.


Utajiri haufai kitu siku ya kasirani, lakini haki inaokoa kutoka kifo.


Mali iliyopatikana kwa njia mbaya haifai, lakini haki inaokoa mutu kutoka kifo.


Yawe ameunyoosha mukono wake juu ya bahari amezitetemesha falme; ametoa amri kuharibu makimbilio ya Kanana.


Muji wa Askeloni utaona hayo na kuogopa, nao muji wa Gaza utagaagaa kwa uchungu; hata Ekroni, maana tumaini lake litatoweka. Gaza utapoteza mufalme wake, nao Askeloni hautakaliwa na watu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite