Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




ZAKARIA 9:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Muji wa Tiro umejijengea kuta kubwa, umejilundikia feza kama mavumbi, na zahabu kama takataka katika barabara.

Gade chapit la Kopi




ZAKARIA 9:3
16 Referans Kwoze  

Vitu vyako vilipofika katika inchi za ngambo, ulitimiza mahitaji ya watu wengi! Kwa wingi wa utajiri wa vitu vyako uliwatajirisha wafalme wa dunia.


Hata akilundika feza kama vile mavumbi, na nguo kama vile udongo wa mufinyanzi,


na kufika kwenye ukuta wa muji wa Tiro, wakaingia kwenye miji yote ya Wahivi na ya Wakanana. Kisha, walitoka wakaenda Negebu ya Yuda kule Beri-Seba.


Hapo, mupaka uligeuka kuelekea Rama na kufikia kwenye muji wa Tiro uliokuwa na kuta. Kisha ukageuka kuelekea Hosa na kuishia kwenye bahari ya Mediteranea. Miji mingine iliyokuwa katika eneo lile ni Maharabu, Akizibu,


Ni nani aliyepanga mambo haya juu ya Tiro, muji uliosimika wafalme, wachuuzi wake walikuwa wakubwa, wakaheshimiwa katika dunia yote?


ukitupilia mbali mali yako, ukitupa zahabu ya Ofiri kwenye ukingo wa kijito,


Basi, Solomono alifanya feza katika Yerusalema kuwa kitu cha kawaida kama mawe, na mbao za mierezi zilikuwa nyingi kama mbao za mikuyu ya Shefela.


Vyombo vyote vya kunywa divai vya mufalme Solomono vilikuwa vya zahabu, na vyombo vyote vilivyokuwa katika Nyumba ya Pori ya Lebanoni vilikuwa vya zahabu safi; hakuna kilichotengenezwa kwa feza maana madini ya feza haikuhesabiwa kuwa kitu wakati ule.


Yawe ameunyoosha mukono wake juu ya bahari amezitetemesha falme; ametoa amri kuharibu makimbilio ya Kanana.


Ataunyanganya utajiri wako pamoja na biashara yako. Atazibomoa kuta zako na kuziangusha nyumba zako nzuri; mawe, mbao na udongo ulivyotumia kwa kujenga nyumba hizo watavitupa katika bahari.


Lakini sasa umevunjikia ndani ya bahari; umeangamia katika vilindi vya maji. Biashara yako na watu wote waliokuwa ndani yako vimezama pamoja nawe.


pamoja na wakubwa waliokuwa na zahabu, waliojaza nyumba zao feza tele.


Mali yako, biashara yako, na vitu vyako, waongozi wako wote katika chombo, wafundi wako wa mashua na wachuuzi wako, waaskari wako wote wanaokuwa kwako, pamoja na wasafiri wanaokuwa kwako, vyote vitaangamia ndani ya bahari, siku ile ya kuangamizwa kwako.


Neno la Yawe lilinifikia kusema hivi:


Yawe anasema hivi: Kwa sababu ya makosa matatu ya watu wa Tiro, hata kwa mane, sitageuza nia yangu. Wamekamata watu wengi na kuwapeleka mpaka Edomu. Hawakutii mapatano ya urafiki waliokuwa wamefanya.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite