Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




ZAKARIA 9:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 vilevile muji wa Hamati unaopakana na Hadiraki, na hata miji ya Tiro na Sidona ingawa inajiona kuwa na hekima sana.

Gade chapit la Kopi




ZAKARIA 9:2
20 Referans Kwoze  

Wewe mwanadamu! Imba wimbo wa maombolezo juu ya mufalme wa Tiro. Umwambie kwamba: Bwana wetu Yawe anasema hivi: Wewe mufalme wa Tiro ulikuwa mupaka wa ukamilifu; ulijaa hekima na uzuri kamili.


Hii ni juu ya Damasiki: Miji ya Hamati na Arpadi, imejaa wasiwasi kwa kufikiwa na habari mbaya; mioyo ya watu wake inayeyuka kwa hofu, imefazaika kama bahari isiyoweza kutulia.


Waisraeli wanaokuwa katika uhamisho, lile jeshi la Waisraeli, watarizi inchi ya Foinikia mpaka Zerepata. Watu wa Yerusalema wanaokuwa katika uhamisho kule Sefaradi watarizi miji ya Negebu.


Enyi Waisraeli, kweli nitaleta taifa moja likuje kuwashambulia. –Ni ujumbe wa Yawe.– Nalo litawatesa ninyi kuanzia Hamati upande wa kaskazini, mpaka kwenye kijito cha Araba, upande wa kusini.


Mufalme Nebukadneza wa Babeli akawapiga na kuwaua watu hao kule Ribla katika inchi ya Hamati. Hivyo watu wa Yuda wakapelekwa kuwa watumwa inje ya inchi yao.


Kusudi asiendelee kutawala akiwa kule Yerusalema, Neko mufalme wa Misri alimufunga kule Ribla katika inchi ya Hamati, akawalipisha watu wa Yuda kodi ya kilo elfu tatu na mia ine za feza na kilo makumi tatu na ine za zahabu.


“Ondoka uende katika muji wa Zerepata, karibu na Sidona, ukae kule. Nimemwamuru mujane mumoja akupatie chakula kule.”


Basi, watu hao wakaenda na kupeleleza inchi toka jangwa la Sini mpaka Rehobu, karibu na njia ya kuingilia Hamati.


wafalme wote wa Tiro na Sidona; wafalme wa inchi zinazokuwa kandokando ya bahari ya Mediteranea;


Hiyo ni siku ya kuwaangamiza Wafilistini wote, kukomesha musaada uliobakia kutoka Tiro na Sidona. Maana Yawe anawaangamiza Wafilistini, watu waliobaki wa kisanga cha Kafutori.


Kutoka hapo utaendelea mpaka Berota na Sibraimu (unaokuwa kati ya Damasiki na Hamati), na mpaka muji wa Hazori-Hatikoni unaokuwa katika inchi ya Haurani.


Neno la Yawe lilinifikia kusema hivi:


Neno la Yawe lilinifikia kusema hivi:


Yawe anasema hivi: Kwa sababu ya makosa matatu ya watu wa Damasiki, hata kwa mane, sitageuza nia yangu. Wamekatakata watu wa Gileadi wakitumia majembe ya mashini ya kulima.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite