Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




ZAKARIA 9:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Wakati ule, Yawe, Mungu wao, atawaokoa, maana wao ni kundi lake; nao watangaa katika inchi yake kama mawe ya bei kali katika taji.

Gade chapit la Kopi




ZAKARIA 9:16
25 Referans Kwoze  

Utakuwa taji zuri katika mukono wa Yawe; taji la kifalme katika mukono wa Mungu wako.


“Musiogope ninyi kundi dogo! Kwa kuwa Baba yenu amependelea kuwapa ninyi ule Ufalme wake.


Siku hiyo, nitakutwaa wewe Zerubabeli mwana wa Saltieli, mutumishi wangu. –Ni ujumbe wa Yawe wa majeshi! Nitakusimika utawale kwa jina langu. –Ni ujumbe wa Yawe! Wewe ndiwe niliyekuchagua. –Ni ujumbe wa Yawe wa majeshi!


Kondoo wangu wanasikia sauti yangu, ninawajua, nao wananifuata.


Nanyi, ee kondoo wangu, ninyi ni watu wangu, nami ni Mungu wenu. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.


Maana mimi Yawe nimemukomboa Yakobo, nimemwokoa kutoka kwa wenye nguvu kuliko yeye.


Wazao wa wale waliokutesa, watakuja na kuinama uso mpaka chini mbele yako. Wote wale waliokuzarau, watapiga magoti kwenye miguu yako. Watakuita: “Muji wa Yawe”, “Sayuni”, “Muji wa Mutakatifu wa Israeli”.


Mataifa watatembea katika mwangaza wako, wafalme watavutwa na kungaa kwako.


Mujue kwamba Yawe ndiye Mungu. Yeye ndiye aliyetuumba, sisi ni mali yake; sisi ni watu wake na kondoo wake anaowachunga.


Yawe wa majeshi anasema hivi: Wakati ule, watu kumi kutoka mataifa ya kila luga watamukamatilia Muyuda mumoja na kushika nguo yake na kumwambia: Tunataka kwenda pamoja nanyi, kwa sababu tumesikia kwamba Mungu yuko pamoja nanyi.


Bwana wetu Yawe anakuja na nguvu, kwa mukono wake anatawala. Yeye anakuja na mapato yake, anafika na mushahara wake.


Wakati huo nitawakusanya, na kuwafanya mujulikane na kusifiwa kati ya watu wote katika dunia, na kuwarudishia hali yenu njema, nanyi mutaona kwa macho yenu wenyewe. –Ni Yawe anayesema hivyo.


Ee Mungu, uwachunge watu wako kwa fimbo yako, uwachunge wale wanaokuwa kundi lako mwenyewe ambao wanaishi peke yao katika pori na kuzungukwa na inchi yenye mboleo. Uwachunge kama ulivyofanya pale zamani katika shamba la malisho ya Basani na Gileadi.


Kisha, nitawakusanya kondoo wangu waliobaki kutoka inchi zote nilipowafukuza, na kuwarudisha katika malisho yao. Nao watazaa na kuongezeka.


Yeye ndiye atakayeleta amani. Waasuria wakishambulia inchi yetu, na kuingia katika nyumba zetu nzuri, tutatuma walinzi wetu wapigane nao, tutawapeleka waongozi wetu kwa wingi.


Enyi mataifa, musikilize neno langu mimi Yawe, mulitangaze katika visanga vya mbali, museme hivi: Aliyemusambaza Israeli, atamukusanya, atamutunza kama muchungaji anavyotunza kondoo wake.


Nitawaimarisha watu wa Yuda; nitawaokoa wazao wa Yosefu. Nitawarudisha kwao kwa maana ninawaonea huruma, nao watakuwa kama vile sikuwa nimewakataa. Mimi ni Yawe, Mungu wao, nami nitayasikiliza maombi yao.


Kisha utatwaa mawe mawili ya sardoniki ambayo utachora juu yake majina ya wana wa Israeli.


Basi, kutakuwa mawe kumi na mawili yaliyochorwa majina kumi na mawili ya wana wa Israeli. Kila moja litakuwa kama muhuri, kwa kusimamia makabila yale kumi na mawili.


Minara yako nitaijenga kwa mawe ya akiki, milango yako kwa almasi, na ukuta wako kwa mawe ya bei kali.


Basi, Bwana wetu Yawe anasema hivi: Mimi mwenyewe nitawatafuta kondoo wangu na kuwatunza.


Kama muchungaji anavyowatafuta kondoo wake waliosambazwa, ndivyo nitakavyowatafuta kondoo wangu. Nitawarudisha kutoka kila pahali waliposambazwa kwa siku yenye mawingu ya hatari na giza nene.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite