Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




ZAKARIA 9:15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

15 Yawe wa majeshi atawalinda watu wake, nao watawaangamiza waadui zao. Watapiga kelele katika vita kama walevi, wataimwanga damu ya waadui zao. Itatiririka kama damu ya nyama wanaotolewa kwa sadaka iliyomiminwa juu ya mazabahu kutoka ndani ya bakuli.

Gade chapit la Kopi




ZAKARIA 9:15
25 Referans Kwoze  

Siku hiyo, nitawafanya wakubwa wa Yuda kuwa kama chungu chenye moto mukali katika pori, kama mwenge wa moto unaowaka kati ya miganda. Watayateketeza mataifa yote yanayokuwa kandokando yao. Lakini watu wa Yerusalema wataendelea kuishi salama katika muji wao.


Watu wa Efuraimu watakuwa kama mashujaa katika vita; watajaa furaha kama watu waliokunywa divai. Watoto wao wataona hayo na kufurahi, watajaa furaha ndani ya moyo kwa sababu yangu mimi Yawe.


Siku hiyo, mimi Yawe nitawalinda wakaaji wa Yerusalema. Wanaokuwa wazaifu zaidi kati yao watakuwa na nguvu kama mufalme Daudi. Wazao wa Daudi watashika usukani kwa kuwaongoza watu wa Yuda kama Mungu, au kama malaika wa Yawe.


Watu wa Yuda watakuwa kama mashujaa katika vita, watawakanyaga waadui zao ndani ya matope katika njia. Watapigana kwa sababu mimi Yawe nipo pamoja nao; nao watawafezehesha hata waaskari wapanda-farasi.


Katika kila pembe ya mazabahu ile utatengeneza upembe ambao utakuwa umeundwa kutokana na mazabahu yenyewe. Mazabahu ile yote utaipakaa shaba.


Kisha Bwana aliamuka kama kutoka katika usingizi, kama shujaa aliyechangamushwa na divai.


Kuhani atachovya kidole chake katika damu ya sadaka kwa ajili ya zambi na kuipakaa kwenye pembe za mazabahu ya kuteketezea sadaka. Damu inayobaki ataimwanga chini kwenye tako la mazabahu ya kuteketezea sadaka.


Kisha, sehemu ya damu atazipakaa kwenye pembe za mazabahu inayokuwa katika hema la mukutano mbele ya Yawe. Damu inayobaki ataimwanga chini kwenye tako la mazabahu ya kuteketezea sadaka inayokuwa karibu na mulango wa hema la mukutano.


Musilewe divai kwa maana inaleta upotovu, lakini mujazwe na Roho.


Hivi, mahubiri ya kufa kwa Kristo juu ya musalaba yanahesabiwa kuwa upumbafu kwa wale wanaopotea. Lakini kwa sisi tunaookolewa ni uwezo wa Mungu.


Wakati ule, kwenye kengele za farasi kutaandikwa maandiko haya: “Vimetolewa kwa Yawe.” Vyungu vinavyokuwa katika hekalu la Yawe vitakuwa kama mabakuli yanayokuwa mbele ya mazabahu.


Angalia jinsi gani uzuri na urembo wake unavyokuwa! Vijana wanaume na wanawake watastawi kwa wingi wa ngano na divai mupya.


Waisraeli watawashinda waadui zao na kuwaangamiza kabisa.


Ee ninyi wote wenye kiu mukuje kwenye maji! Mukuje, wote hata musiokuwa na feza; mununue chakula na mupate kula, mununue divai na maziwa. Bila feza, bila malipo!


Nilisema nitapanda muti wa ngazi na kuchuma shada za ngazi. Kwangu maziba yako ni kama shada za zabibu, harufu nzuri ya pumzi yako ni kama matunda ya mutofaa;


Ninaingia katika bustani yangu, dada yangu, muchumba wangu. Ninakusanya manemane na majani yenye harufu, ninakula sega langu la asali, ninakunywa divai yangu na maziwa yangu. Mukule, enyi warafiki, mukunywe; mukunywe sana, wapendwa wangu.


Unipeleke, tuende haraka, mufalme amenileta katika chumba chake. Tutafurahi na kukushangilia pamoja, tutasifu mapenzi yako kuliko divai. Wabinti wana haki ya kukupenda!


Lakini Daudi akamwambia Goliati: “Wewe unanifikia kwa upanga na mikuki. Lakini mimi ninakufikia kwa jina la Yawe wa majeshi, Mungu wa waaskari wa Israeli, ambaye wewe umemutukana.


Kuhani atatwaa sehemu ya damu na kuipakaa kwenye pembe za mazabahu ya kufukizia ubani wenye harufu nzuri, mbele ya Yawe katika hema la mukutano. Damu inayobaki ataimwanga chini kwenye tako la mazabahu ya kuteketezea sadaka inayokuwa karibu na mulango wa hema la mukutano.


Kisha Yawe atatoka na kuyapiga vita mataifa hayo, kama vile anavyofanya siku zote wakati wa vita.


Yawe anasema kwamba yeye mwenyewe atakuwa ukuta wa moto kwa kuulinda muji huo pande zote, naye atakaa mule kwa utukufu wake.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite