Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




ZAKARIA 9:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Yuda nitamutumia kama upinde wangu; Efuraimu nimemufanya mushale wangu. Ee Sayuni, watu wako nitawatumia kama upanga kwa kuwashambulia watu wa Ugriki; watakuwa kama upanga wa shujaa.

Gade chapit la Kopi




ZAKARIA 9:13
31 Referans Kwoze  

Watapigana vita na Mwana-Kondoo, lakini Mwana-Kondoo pamoja na waaminifu wake aliowaita na kujichagulia atawashinda, kwa sababu yeye ni Bwana wa wabwana na Mufalme wa wafalme.”


Alifanya maneno yangu kuwa makali kama upanga mukali, alinificha katika kivuli cha mukono wake; aliufanya ujumbe wangu kuwa mukali kama chongo ya mushale, akanificha kama mushale ndani ya mufuko wake.


Wewe ni muzuri kuliko wanadamu wote, maneno yako ni rehema tupu, Mungu amekubariki milele.


Na wale waliobaki wakauawa kwa upanga uliotoka katika kinywa cha yule aliyepanda juu ya yule farasi. Ndege wote wakashibishwa na kula nyama za miili yao.


Ndani ya kinywa chake mulitoka upanga mukali kwa kushinda mataifa. Naye atatawala kwa fimbo ya chuma na kukamua zabibu ndani ya kikamulio cha divai kinachojaa kasirani kali ya Mungu Mwenye Uwezo.


“Umwandikie malaika wa kanisa la Pergamo hivi: “Ujumbe huu unatoka kwa yule anayekuwa na upanga wenye makali ngambo zote mbili.


Alikuwa ameshika nyota saba katika mukono wake wa kuume. Ndani ya kinywa chake mulitoka upanga wenye makali ngambo zote mbili, uso wake ulingaa sana kama jua wakati linapopiga vikali sana.


Kwa maana Neno la Mungu ni lenye uzima, na lina nguvu; ni kali kupita upanga unaokata ngambo mbili. Linapenya hata linatenga moyo na roho na hata viungo na ubongo. Nalo linatambua nia na mawazo ya mutu.


Nimeshindana vizuri, nimekimbia na kufika mwisho wa mashindano yangu. Nimelinda imani yangu.


Mupokee wokovu kama vile kofia ya chuma ya kuwalinda, na Neno la Mungu kama upanga munaopewa na Roho.


Wakombozi watapanda juu ya mulima Sayuni kwa kuutawala mulima wa wazao wa Esau; naye Yawe atakuwa ndiye Mufalme.


Nilichagua manabii kati ya wana wenu, na wengine kati ya vijana wenu kuwa wanaziri. Enyi Waisraeli, haya ninayosema si ya kweli? –Ni ujumbe wa Yawe.–


Watoto wa Sayuni waliosifiwa sana, waliokuwa na bei kama zahabu safi, namna gani sasa wamekuwa kama vyombo vya udongo, kazi ya mikono ya mufinyanzi!


Yawe anasema hivi: Wewe Babeli ni nyundo na silaha yangu ya vita; ninakutumia kwa kuyavunjavunja mataifa, ninakutumia kwa kuangamiza falme.


Wamusifu Mungu kwa sauti kubwa, wakishika panga zenye kukata pande mbili,


Zaburi ya Daudi. Atukuzwe Yawe, yeye ni: nguvu yangu, yule anayeizoeza mikono yangu kupigana vita na kuvifundisha vidole vyangu kugombana,


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite