Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




ZAKARIA 9:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Ujumbe wa Yawe: Neno la Yawe ni juu ya azabu ya miji Hadiraki na Damasiki. Maana inchi ya Aramu ni mali ya Yawe, kama vile makabila yote ya Israeli yanavyokuwa,

Gade chapit la Kopi




ZAKARIA 9:1
22 Referans Kwoze  

Ujumbe wa neno la Yawe lililowafikia Waisraeli kwa njia ya Malaki.


Yawe wa majeshi anasema kwamba yeye mwenyewe ataipeleka laana hiyo. Itapenya kila nyumba ya mwizi na kila nyumba ya mwenye kuapa uongo kwa kutumia jina lake; itakaa mule na kuteketeza nyumba hiyo yote, mbao na mawe.


Yawe, anasema hivi: Kama vile muchungaji anavyonyanganya toka katika kinywa cha simba miguu miwili tu au kipande cha sikio la kondoo, ndivyo watu wachache tu wa Israeli wanaoishi Samaria, ambao sasa wanalalia vitanda vizuri na matandiko ya hariri watakavyobaki.


Ee Yawe! Wewe ndiwe nguvu yangu na upango wangu; wewe ni kimbilio langu wakati wa taabu. Mataifa toka pande zote za dunia yatakufikia na kusema: Miungu ya babu zetu ilikuwa ya uongo, ilikuwa ya bure, isiyofaa kitu.


Yawe ameonyesha nguvu yake tukufu, mbele ya mataifa yote. Atawaokoa watu wake, na ulimwengu wote utashuhudia.


Haya ni maono, ambayo nabii Isaya mwana wa Amozi, aliyofunuliwa na Mungu juu ya inchi ya Babeli:


Viumbe vyote vinakutazamia, nawe unavipatia chakula chao kwa wakati wake.


Ninainua macho kwa Yawe siku zote; yeye ataopoa miguu yangu kutoka mutego.


Wewe ndiwe Mungu wetu! Uwaazibu, maana sisi hatuna uwezo wowote mbele ya jeshi kubwa kama hili linalotufikia. Hatujui la kufanya lakini tunatazamia musaada kutoka kwako.”


Kule, akagawanya jeshi lake katika makundi. Usiku, akawashambulia waadui zake, akawashinda na kuwafukuza mpaka Hoba, upande wa kaskazini wa Damasiki.


Yawe anasema hivi: Kwa sababu ya makosa matatu ya watu wa Tiro, hata kwa mane, sitageuza nia yangu. Wamekamata watu wengi na kuwapeleka mpaka Edomu. Hawakutii mapatano ya urafiki waliokuwa wamefanya.


Ujumbe wa Mungu juu ya Ninawe. Kitabu cha maono ya Nahumu wa Elkosi.


Wewe unapanga kwa hekima na unafanya maajabu; njia za watu wote ziko wazi mbele yako, unamulipa kila mumoja kadiri ya njia zake na matendo yake.


Maendeleo ya ujenzi wa hekalu yanaonekana madogo, na watu wanayazarau; lakini watamwona Zerubabeli akiendelea kulijenga hekalu, nao watafurahi. Sasa, juu ya hizo taa saba, yule malaika akaniambia: Ni macho saba ya Yawe yanayoona kila nafasi katika dunia.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite