Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




ZAKARIA 8:21 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

21 Wakaaji wa muji mumoja watawaendea wakaaji wa muji mwingine na kuwaambia: Tuende pamoja kumwabudu Yawe wa majeshi na kumwomba baraka!

Gade chapit la Kopi




ZAKARIA 8:21
10 Referans Kwoze  

Watu wa muji wa Beteli walikuwa wamewatuma Sareseri na Regemu-Meleki pamoja na watu wao kumwomba Yawe rehema zake,


Basi tumutambue, tujikaze sana kumujua Yawe. Kuja kwake ni hakika kama mapambazuko, yeye atatufikia kama vile manyunyu, kama vile mvua za kwanza zinavyolowanisha udongo.


Mumusifu Yawe, enyi viumbe vyake vyote; mumusifu popote munapokuwa katika utawala wake. Ee nafsi yangu, umusifu Yawe!


Kweli, mataifa yenye nguvu na watu wengi watakuja Yerusalema kumwabudu Yawe wa majeshi na kumwomba baraka.


Watu wote ambao walikuwa wamekusudia kwa moyo kumwabudu Yawe, Mungu wa Israeli, kutoka katika makabila yote ya Israeli, waliandamana na Walawi mpaka Yerusalema kusudi wapate kumutolea sadaka Yawe, Mungu wa babu zao.


watu wengi wataenda kule na kusema, Mukuje tupandie kwenye mulima wa Yawe, tuende kwenye nyumba ya Mungu wa Yakobo, apate kutufundisha njia zake, nasi tutafuata mapito yake. Maana sheria itakuja kutoka Sayuni; neno la Yawe kutoka Yerusalema.


Maana kutakuja siku ambapo walinzi watalalamika hivi katika vilima vya Efuraimu: Musimame, tupande kwenda Sayuni kwa Yawe, Mungu wetu.


Wale wanafunzi wawili waliposikia maneno yale, wakamufuata Yesu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite