Basi tumutambue, tujikaze sana kumujua Yawe. Kuja kwake ni hakika kama mapambazuko, yeye atatufikia kama vile manyunyu, kama vile mvua za kwanza zinavyolowanisha udongo.
Watu wote ambao walikuwa wamekusudia kwa moyo kumwabudu Yawe, Mungu wa Israeli, kutoka katika makabila yote ya Israeli, waliandamana na Walawi mpaka Yerusalema kusudi wapate kumutolea sadaka Yawe, Mungu wa babu zao.
watu wengi wataenda kule na kusema, Mukuje tupandie kwenye mulima wa Yawe, tuende kwenye nyumba ya Mungu wa Yakobo, apate kutufundisha njia zake, nasi tutafuata mapito yake. Maana sheria itakuja kutoka Sayuni; neno la Yawe kutoka Yerusalema.