Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




ZAKARIA 8:19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

19 Yawe wa majeshi anasema hivi: Siku za mafungo ya kula chakula ya mwezi wa ine, mwezi wa tano, mwezi wa saba na mwezi wa kumi, zitakuwa nyakati za furaha na shangwe; zitakuwa sikukuu za shangwe kwa watu wa Yuda. Basi, mupende ukweli na amani.

Gade chapit la Kopi




ZAKARIA 8:19
27 Referans Kwoze  

Na katika siku ya kenda ya mwezi wa ine, mwaka wa kumi na moja wa utawala wa Zedekia, sehemu ya ukuta wa muji ilibomolewa.


Hivi ndivyo munavyopaswa kufanya: Kila mumoja wenu amwambie mwenzake ukweli. Tribinali zenu zitoe siku zote hukumu za haki zinazoleta amani.


Uwaambie wakaaji wote wa inchi na makuhani hivi: Kwa muda wa miaka makumi saba iliyopita, ninyi mulikuwa mukifunga na kuomboleza katika mwezi wa tano na wa saba. Munazani mulifunga kwa ajili yangu?


na kuwauliza makuhani wa hekalu la Yawe wa majeshi maneno haya: Tuendelee kuomboleza na kufunga kula chakula katika mwezi wa tano kama tulivyofanya kwa muda wa miaka mingi sasa?


Ikakuwa katika siku ya kumi ya mwezi wa kumi, mwaka wa kenda wa utawala wa Zedekia, Nebukadneza mufalme wa Babeli, alifika na waaskari wake wote kuushambulia Yerusalema, wakauzunguka kila upande.


Katika mwezi wa saba, Isimaeli mwana wa Netania, mujukuu wa Elisama, aliyekuwa wa ukoo wa kifalme, akafika kwa Gedalia pamoja na watu kumi, akamushambulia Gedalia, akamwua. Vilevile, akawaua Wayuda na Wababeli waliokuwa naye.


Usikie, ee Yawe, unihurumie; ee Yawe, unisaidie!”


Waliokombolewa na Yawe watarudi, watakuja Sayuni wakipiga vigelegele. Watakuwa wenye furaha ya milele, watajaliwa furaha na shangwe; huzuni na kilio vitatoweka kabisa.


Siku hiyo mutasema: Ninakushukuru, ee Yawe, maana ingawa ulinikasirikia, hasira yako imetoweka, nawe umenifariji.


Wayuda walishinda waadui zao katika siku hizo, na katika mwezi huo huzuni yao iligeuzwa kuwa furaha, na kilio chao kuwa sikukuu. Waliagizwa wakuwe wanazikumbuka siku hizo kwa kufanya karamu na sherehe, kupelekeana zawadi za chakula na kuwapa wamasikini vitu.


Lakini mbali ya muji ule kuna watu wenye kuchukiza, wachawi, wazinzi, wauaji, wanaobudu sanamu na wasema uongo na wote wanaoupenda.


Watu wako uliowakomboa, ee Yawe, watarudia, watakuja Sayuni wakiimba; watajaa furaha ya milele, watapata furaha na shangwe. Huzuni na maombolezo vitatoweka kabisa.


Katika kila jimbo na kila muji, popote pale tangazo hili liliposomwa, Wayuda wakafurahi na kushangilia, wakafanya sherehe na mapumziko; na watu wengine wengi wakajifanya kuwa Wayuda, maana waliwaogopa sana Wayuda.


Lakini kwa siku ya kwanza ya kufunga kula chakula, wewe utakwenda mbele ya watu wote, ndani ya nyumba ya Yawe, usome kitabu chenye maneno ya Yawe uliyoyaandika kutoka katika kinywa changu. Utayasoma maneno hayo mbele ya watu wote wa Yuda waliofika kutoka miji yao vilevile.


Yawe wa majeshi anasema hivi: Nitaurudilia Sayuni na kufanya makao yangu katika Yerusalema. Muji Yerusalema utaitwa “Muji Mwaminifu”, na mulima wa Yawe wa majeshi utaitwa “Mulima Mutakatifu”.


Yawe wa majeshi akanitolea mimi Zakaria ujumbe huu:


Katika siku ya kumi ya mwezi wa kumi, mwaka wa tisa wa utawala wa Zedekia, Nebukadneza mufalme wa Babeli akafika na waaskari wake kwa kushambulia Yerusalema. Akapiga kambi mbele ya muji ule na kujenga ngazi kuuzunguka.


Ujiepushe na uovu, utende mazuri; utafute amani na kuifuatilia.


Katika siku kumi, ya mwezi wa kumi, kwa mwaka wa kenda tangu kuhamishwa kwetu, neno la Yawe lilinifikia kusema hivi:


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite