Yawe wa majeshi anasema hivi: Siku za mafungo ya kula chakula ya mwezi wa ine, mwezi wa tano, mwezi wa saba na mwezi wa kumi, zitakuwa nyakati za furaha na shangwe; zitakuwa sikukuu za shangwe kwa watu wa Yuda. Basi, mupende ukweli na amani.
Yawe wa majeshi anasema hivi: Mujipe moyo! Sasa munayasikia maneno ambayo mulitangaziwa na manabii wakati musingi wa hekalu langu ulipowekwa kulijenga upya.
Roho wa Kristo aliyekuwa ndani yao alitangulia kushuhudia mateso yatakayomupata Kristo na utukufu utakaokuwa nyuma. Nao walijitolea kusudi wapate kuvumbua wakati gani na kwa njia gani mambo haya yatafanyika.